Kwa Habari za kitaifa, Kimataifa, Michezo, Burudani,Uchambuzi na matangazo. Matukio Daima Blog, Ni yetu Sote!
WATU WENYE SILAHA WAUA WATU 11 KATIKA UWANJA WA MPIRA MEXICO

WATU WENYE SILAHA WAUA WATU 11 KATIKA UWANJA WA MPIRA MEXICO

 

Kundi la washambuliaji wenye silaha limewaua watu 11 na kuwajeruhi 12 katika uwanja wa soka baada ya mechi katika jiji la Salamanca huko Mexico, amesema meya Cesar Prieto, kwenye Facebook siku ya Jumapili.

Prieto aliongeza kuwa mwanamke na mtoto ni miongoni mwa waliojeruhiwa katika shambulio la "kusikitisha" dhidi ya jamii ya Loma de Flores.

Uchunguzi umeanzishwa kuhusu shambulio hilo, imesema ofisi ya mwanasheria mkuu katika jimbo la Guanajuato.

"Wale waliohusika watapatikana," Prieto aliongeza katika maelezo yake ya Facebook.

Bado haijafahamika sababu ya shambulio hilo lakini Guanajuato ni mojawapo ya majimbo hatari zaidi nchini Mexico.


Sponsored ads

Mid 1

Mid2

Ad3