TANZIA :MWANAHABARI MKONGWE NCHINI LEONARD MWAKALEBELA AFARIKI DUNIA
Jul 8, 2026
Na Matukio Daima Media
Mwandishi Wa Habari Mwandamizi wa Kampuni ya Magazeti ya Serikali (TSN), Leonard Wilfred Mwakalebela, amefariki dunia leo Julai 8 nyumbani kwake, Mnazi Mmoja, Dar es Salaam.
Taarifa zilizotolewa na TSN zinaeleza kuwa Mwakalebela alikuwa akihudumu katika Kurugenzi ya Habari na kwamba taratibu za mazishi zinaendelea kuratibiwa kwa kushirikiana na familia.
Matukio Daima Media inaungana na wanahabari wote Tanzania ,rafiki na wafanyakazi wenzake wote kutoa pole kwa familia ya marehemu.
Taarifa zaidi tutaendelea kuwajiza itoshe kusema tulimpenda sana Leonard Mwakalebela ila Mungu kampenza zaidi yetu hivyo tusema Bwana ametoa na yeye ametwaa jina lake lizidi kuhimidiwa .
AMEN
