UN YASHANGAZWA NA ONGEZEKO LA MAUAJI YA WATU IRAN
Mkuu wa haki za binadamu katika Umoja wa Matafa amesema ameshangazwa na ongezeko la mauaji Iran, huku adhabu kali ikiendelea kutekelezwa, kuwatia hofu watu na kukandamiza upinzani.
Volker Türk alisema kuwa takriban watu 56 wameuawa kwa kunyongwa kutokana na mashtaka yanayohusiana na usalama wa taifa tangu tarehe 19 Machi, wakiwemo watu 27 katika kesi zilizohusishwa na maandamano ya nchi nzima dhidi ya serikali yaliyofanyika mwezi Januari.
Aliongeza kuwa zaidi ya watu wengine 100 wako katika hatari ya kunyongwa kwa mashtaka kama hayo, huku mauaji ya kisheria kwa makosa yanayohusiana na dawa za kulevya pia yakiendelea kwa kasi ya kutisha.
Iran inaaminika kuwa nchi ya pili duniani kwa idadi kubwa zaidi ya utekelezaji wa hukumu za kifo baada ya China. Mwaka jana, ilitekeleza hukumu ya kifo kwa angalau watu 2,159, kulingana na shirika la Amnesty International.
Shirika hilo la haki za binadamu lilisema kuwa hiyo ndiyo idadi kubwa zaidi kuwahi kurekodiwa tangu mwaka 1981, na ilijumuisha mauaji ya watu 45 waliotuhumiwa kuwa wapinzani wa serikali kwa makosa yanayohusiana na usalama wa taifa.
Wanaharakati wameonya kuwa mamalaka za Iran zitatumia zaidi hukumu ya kifo dhidi ya wapinzani kufuatia maanadamano ya Januari, ambapo maelfuya waandamanji waliuawa na makumi ya maelfu kukamatwa.
Mkuu wa haki za binadamu katika Umoja wa Matafa amesema ameshangazwa na ongezeko la mauaji Iran, huku adhabu kali ikiendelea kutekelezwa, kuwatia hofu watu na kukandamiza upinzani.
Volker Türk alisema kuwa takriban watu 56 wameuawa kwa kunyongwa kutokana na mashtaka yanayohusiana na usalama wa taifa tangu tarehe 19 Machi, wakiwemo watu 27 katika kesi zilizohusishwa na maandamano ya nchi nzima dhidi ya serikali yaliyofanyika mwezi Januari.
Aliongeza kuwa zaidi ya watu wengine 100 wako katika hatari ya kunyongwa kwa mashtaka kama hayo, huku mauaji ya kisheria kwa makosa yanayohusiana na dawa za kulevya pia yakiendelea kwa kasi ya kutisha.
Iran inaaminika kuwa nchi ya pili duniani kwa idadi kubwa zaidi ya utekelezaji wa hukumu za kifo baada ya China. Mwaka jana, ilitekeleza hukumu ya kifo kwa angalau watu 2,159, kulingana na shirika la Amnesty International.
Shirika hilo la haki za binadamu lilisema kuwa hiyo ndiyo idadi kubwa zaidi kuwahi kurekodiwa tangu mwaka 1981, na ilijumuisha mauaji ya watu 45 waliotuhumiwa kuwa wapinzani wa serikali kwa makosa yanayohusiana na usalama wa taifa.
Wanaharakati wameonya kuwa mamalaka za Iran zitatumia zaidi hukumu ya kifo dhidi ya wapinzani kufuatia maanadamano ya Januari, ambapo maelfuya waandamanji waliuawa na makumi ya maelfu kukamatwa.