RAIS SAMIA ARIDHIA OMBI LA DKT. NCHIMBI KUJIUZULU
Aug 25, 2026
NA MATUKIO DAIMA MEDIA
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amepokea rasmi barua ya ombi la kujiuzulu kwa Makamu wa Rais, Balozi Dkt. Emmanuel John Nchimbi, na kuridhia ombi hilo.
Kwa mujibu wa taarifa kwa umma iliyotolewa leo, Agosti 25, 2026, na Ofisi ya Katibu Mkuu Kiongozi, Dkt. Nchimbi ameomba kujiuzulu katika nafasi hiyo kuanzia Septemba 4, 2026.
Taarifa hiyo imeeleza kuwa Rais Samia ameridhia ombi hilo na kwamba taratibu za kikatiba za kumpata Makamu wa Rais mwingine zitachukuliwa.
Taarifa hiyo imesainiwa na Balozi Dkt. Moses M. Kusiluka, Katibu Mkuu Kiongozi.

