Kwa Habari za kitaifa, Kimataifa, Michezo, Burudani,Uchambuzi na matangazo. Matukio Daima Blog, Ni yetu Sote!
KIJANA (19) AHUKUMIWA MWAKA 01 JELA KISA KUWATUSI VIONGOZI KUPITIA TIKTOK

KIJANA (19) AHUKUMIWA MWAKA 01 JELA KISA KUWATUSI VIONGOZI KUPITIA TIKTOK

 


NA MATUKIO DAIMA MEDIA ,MBEYA

Mahakama ya Mwanzo Mbeya mjini imemhukumu kifungo cha mwaka mmoja jela Ramadhan Rudabuka (19) DJ na mkazi wa Patamela Wilayani Chunya baada ya kutiwa hatiani kwa kosa la kusambaza maudhui yasiyofaa katika mtandao wa TIKTOK.


Hukumu hiyo imetolewa mbele ya Hakimu wa Mahakama ya Mwanzo Mbeya mjini Ayubu Shirima.


Ilielezwa kuwa mshitakiwa alijirekodi na kusambaza maudhui yasiyofaa kwa kutoa lugha ya matusi dhidi ya viongozi wa Serikali kwa lengo la kupata wafuasi wengi katika akaunti yake ya TIKTOK licha ya kukataa kutenda kosa lakini ushahidi uliithibitishia Mahakama mshtakiwa kutenda kosa hilo.


Baada ya hapo ndio Hakimu wa Mahakama ya mwanzo Mbeya mjini alitoa adhabu kwa kijana huyo mwenye umri wa miaka 19 kwenda kutumikia kifungo cha miezi 12 jela ili iwe fundisho kwake na watu wengine wenye tabia kama hiyo hasa katika mitandao ya kijamii nchini.


Sponsored ads

Mid 1

Mid2

Ad3