MAJI CF YATUPA ULAJI MWINGI – WAJASIRIAMALI IRINGA
NA MATUKIO DAIMA MEDIA, IRINGA
BAADHI ya wafanyabiashara wadogo mjini Iringa wamesema wamehamasika kuuza maji ya CF yanayozalishwa wilayani Mufindi, mkoani Iringa, kutokana na kupata faida nzuri pamoja na mwitikio mkubwa wa wateja wanaonunua maji hayo.
Wakizungumza na Matukio Daima Media, wafanyabiashara hao, Salima Abdalah Alli, Wema Kalinga na Keni Sanga, wamesema maji ya CF yameendelea kupata soko katika maeneo mbalimbali ya mjini Iringa, hali inayowafanya kuongeza kiwango cha bidhaa hiyo katika biashara zao.
Wafanyabiashara hao wameipongeza kampuni inayozalisha maji ya CF kwa kuweka mazingira mazuri ya biashara kwa wauzaji pamoja na kuhakikisha bidhaa hiyo inawafikia kwa wakati.
Wamesema moja ya sababu zinazowavutia kuendelea kuuza maji hayo ni bei yake ya jumla, ambayo inawawezesha kupata faida nzuri wanapouza kwa wateja wao.
Kwa mujibu wa wafanyabiashara hao, katoni ya maji ya CF hununuliwa kwa bei ya jumla ya Shilingi 3,800, huku katoni ya chupa kubwa ikiuzwa kwa Shilingi 4,000, bei ambayo wamesema inawapa nafasi nzuri ya kupata faida katika biashara zao.
Wamesema katika biashara ya maji, bei ya jumla ina mchango mkubwa katika kuamua kiwango cha faida anachopata mfanyabiashara, hivyo bei ya maji ya CF imekuwa moja ya sababu zinazowafanya wafanyabiashara wengi kuyapokea vizuri.
Mbali na suala la bei, wafanyabiashara hao wamepongeza mfumo wa usambazaji wa maji hayo, wakisema magari ya kampuni yamekuwa yakifika mara kwa mara katika maeneo yao kuhakikisha hawakosi bidhaa.
Wamesema katika baadhi ya maeneo magari ya usambazaji yamekuwa yakifika zaidi ya mara tatu kwa siku kulingana na mahitaji, jambo ambalo limewasaidia kukidhi ongezeko la wateja wanaotafuta maji hayo.
Kwa upande wao, baadhi ya watumiaji wa maji ya CF wamesema wamevutiwa na bidhaa hiyo kutokana na ubora wake pamoja na namna ilivyopokelewa katika soko.
Perida Sanga, mmoja wa watumiaji wa maji hayo, amesema kwa sasa maji ya CF yameanza kutumika katika matukio mbalimbali ya kijamii, yakiwemo harusi, misiba, mikutano na sherehe nyingine.
Amesema katika baadhi ya harusi na shughuli mbalimbali, waandaaji wamekuwa wakiyapa maji hayo kipaumbele kutokana na mahitaji na mapendeleo ya wageni.
“Kwa sasa ukienda kwenye matukio mbalimbali kama harusi na misiba unakutana na maji ya CF. Watu wengi wameanza kuyapenda na kuyatumia, jambo ambalo linaonesha jinsi yalivyopokelewa vizuri sokoni,” amesema Perida.
Wafanyabiashara hao wamesema kuongezeka kwa idadi ya watumiaji ni fursa kwa wafanyabiashara wadogo, kwa sababu bidhaa inapokuwa na wateja wengi huwa rahisi kuuzwa na kuwapatia kipato.
Aidha, wameiomba kampuni kuendelea kudumisha ubora wa maji, bei rafiki kwa wafanyabiashara pamoja na mfumo mzuri wa usambazaji ili kuhakikisha bidhaa hiyo inapatikana kwa urahisi katika maeneo mbalimbali.
Walisema bei ya chupa ndogo ya maji ni rafiki zaidi kwa ni Tsh 500 wakati chupa kubwa ni Tsh 10000 bei ambayo ni nzuri .
Maji CF ni maji yenye madini asili yanayotoka katika vyanzo salama vya asili vilivyopo wilayani Mufindi, mkoani Iringa, na kwa sasa yanasambazwa katika maeneo mbalimbali nchini.
Kwa mawasiliano kuhusu maji ya CF, wateja na wafanyabiashara wanaweza kupiga simu +255 762 123 736 au kuwasiliana kupitia barua pepe iliyotolewa na kampuni: cfcompany100@gma.

