Kwa Habari za kitaifa, Kimataifa, Michezo, Burudani,Uchambuzi na matangazo. Matukio Daima Blog, Ni yetu Sote!
POLISI ZIMBABWE WAONYA KUWA KUCHOCHEA VURUGU HAKUTAVUMILIWA

POLISI ZIMBABWE WAONYA KUWA KUCHOCHEA VURUGU HAKUTAVUMILIWA

 

Polisi nchini Zimbabwe wamewaonya wananchi dhidi ya kuchochea ghasia na vitisho kwenye mitandao ya kijamii huku mswada wa kuongeza muda wa Rais Emmerson Mnangagwa ukisomwa kwa mara ya pili bungeni, Jumanne.

Polisi waliweka kizuizi njiani kuelekea bungeni mswada huo ukisomwa kwa mara ya pili katika Bunge la Kitaifa.

Sheria inayopendekezwa itaongeza mihula ya urais na wabunge kwa miaka miwili na kufutwa kwa kura ya moja kwa moja ya urais kupigwa na umma.

Waziri wa sheria alitetea mswada huo unaolenga kuongeza muhula wa urais na kufuta kura ya moja kwa moja ya urais akisema italeta utulivu wa kisiasa.

Wakosoaji wanasema mapendekezo hayo ni kinyume cha sheria na yanadhoofisha demokrasia.

Kundi la wapiganaji wa zamani wa vita vya ukombozi, mashirika ya kiraia na wananchi wamewasilisha changamoto za kisheria kuzuia mswada huo.

Hata hivyo inatarajiwa kupitia Mabunge yote mawili ambapo chama tawala cha Zanu PF kinashikilia zaidi ya thuluthi mbili ya wabunge.

Sponsored ads

Mid 1

Mid2

Ad3