Kwa Habari za kitaifa, Kimataifa, Michezo, Burudani,Uchambuzi na matangazo. Matukio Daima Blog, Ni yetu Sote!
WAUMINI WA KIISILAM WASHAURIWA KUSHIRIKI IBADA YA KUCHINJA NA KUSAIDIA  WENYE UHITAJI

WAUMINI WA KIISILAM WASHAURIWA KUSHIRIKI IBADA YA KUCHINJA NA KUSAIDIA WENYE UHITAJI

 

NA MATUKIO DAIMA MEDIA.

IRINGA.WAUMINI wa kiisilamu nchini wameshauriwa kushiriki Katika ibada ya kuchinja ibada inayoambatana na siku tukufu ya Eid ya Kuchinja na kutoa sadaka kwa wale wasiojiweza kupata kitoweo katika siku hii ya sikukuu.


Wito umetolewa katibu Mkuu wa Taasisi ya DHI-Nureyn Islamic Foundation Sheikh Shams Elmi na kusema kuwa Eid ya kuchinja ilianzishwa na Nabii Ibrahim na mtoto wake Ismail kwa kutoa muhanga uchinjaji wa wanyama na kutoa sadaka kwa Mwenyezi Mungu

Shams alisema kuwa Leo wamechinja Ng’ombe 30 kutoka kwa wafadhili mbalimbali wa ndani ambao wametekeleza ibada kwa kuchinja mifugo hii ili kurudisha kwa Mwenyezi Mungu kwa lengo la kuwasaidia waumini ili waweze kufurahia Eid ya kuchinja kwa furaha kwa kuwapatia kitoweo siku ya leo.

“Sasa hivi tunakagua usalama wa nyama kwa ajili ya kuzifikisha kwa walengwa maeneo tunakayogawa ni vituo vya yatima,nyumba za wajane,maeneo ya walemavu na tutaangalia wale wenye hali ngumu katika maisha na kuwapelekea nyama hizi ikiwa ni sadaka kutoka kwa waislamu”alisema

Aidha Shams alitoa wito kwa waumini wa dini hiyo kuwa ibada ya kuchinja imesisitizwa katika vitabu vya dini nan i ibada inayokusudiwa kumuingizia furaha tu ambaye hana uwezo wa kupata kitoweo siku hii ya Eid.

“Ni wito kwa jamii yote kwa ujumla kwa kuwa hali ya kiuchumi duniani imeathirika kwa kiwango kikubwa sana unapojihimiza kutoa sadaka, kuwasaidia watu kwa njia yeyote ni jambo la heri na kuwapunguzia watu ukali wa maisha”alisema

Alisema kuwa dunia nzima imeathirika kiuchumi awali walikuwa na uwezo wa kuchinja ng’ombe 60 lakini mwaka huu wamechinja ng’ombe 30 kwa sababu ya wafadhili wamerudi nyumba kutokana na hali ya kiuchumi kupanda.

“Hii ni fursa ya kujikumbusha umuhimu wa amani duniani na kuacha kushabikia masuala ya vita, bila kujua atahari zake,vita vinavyotea sasa hivi mashariki ya kati, Israel na Marekani na Iran na maeneo mengine athari zinakuja kwetu mafuta yanapanda bei,na mafuta ndio kila kitu na kusababisha kila bidhaa kupanda bei ni wakati mzuri wa watanzania kuombea amani na usalama kwa mataifa mengine duniani”alisema

Kwa upande wake Masood Daud Masood Imamu wa msikiti wa Dhi- Nureyn amewashukuru wale wote waliojitolea kutoa sadaka hiyo ya ng’ombe wamepokea na kuomba wadau wengine waweze kuwasapoti.

“Taaasisi ya Dhi-nureyn ni taasisi inayosaidia watu wasiojiweza lakini pia yatima,hivyo tunaomba wadau waweze kujitokeza kutusaidia kwa mahitaji mbalimbali na kusaidia jamii na waislamu kwa ujumla”alisema

MWISHO.

 

 

Sponsored ads

Mid 1

Mid2

Ad3