Kwa Habari za kitaifa, Kimataifa, Michezo, Burudani,Uchambuzi na matangazo. Matukio Daima Blog, Ni yetu Sote!
MGOMO WA USAFIRI WAANZA KENYA KUPINGA BEI YA MAFUTA

MGOMO WA USAFIRI WAANZA KENYA KUPINGA BEI YA MAFUTA

 

Raia wengi nchini Kenya wamejikuta wakipata ugumu wa kufika kwenye maeneo yao ya kazi asubuhi ya leo baada ya wamiliki wa mabasi ya abiria pamoja na waendesha bodaboda kuanza mgomo wa kushinikiza serikali kushusha bei ya mafuta.

Waandaaji wa mgomo huo wanasema ongezeko la gharama za mafuta limeendelea kuongeza ugumu wa maisha kwa wananchi wa kawaida. Aidha, wametaka mamlaka ya udhibiti wa nishati na mafuta, EPRA, kuvunjwa wakidai imeshindwa kudhibiti bei hizo.

Mbali na sekta ya uchukuzi wa umma, shughuli za usafirishaji wa mizigo na utalii pia zinatarajiwa kuathirika kutokana na mgomo huo unaoendelea katika maeneo mbalimbali nchini humo.

Mgomo huo umeanza siku chache baada ya wahudumu wa usafiri wa umma kutangaza kuongeza nauli kwa asilimia 50 kufuatia bei mpya za mafuta zilizotangazwa Mei 14.

Kwa sasa, lita moja ya petroli jijini Nairobi inauzwa kwa shilingi 214.25 huku dizeli ikiuzwa kwa shilingi 242.92.

Sponsored ads

Mid 1

Mid2

Ad3