Kwa Habari za kitaifa, Kimataifa, Michezo, Burudani,Uchambuzi na matangazo. Matukio Daima Blog, Ni yetu Sote!
BENDERA YA ISRAEL YAPEPERUSHWA KATIKA MSIKITI WA AL AQSA

BENDERA YA ISRAEL YAPEPERUSHWA KATIKA MSIKITI WA AL AQSA

 

Waziri wa Usalama wa Kitaifa wa mrengo wa kulia nchini Israel, Itamar Ben-Gvir, amevunja utaratibu wa muda mrefu unaohusu maeneo ya ibada ya dini tofauti katika eneo hilo baada ya kupeperusha bendera ya Israel karibu na Msikiti wa Al Aqsa.

Video zilizochapishwa zinaonyesha waziri huyo akiinua bendera ya Israel huku wimbo wenye maneno “Msikiti mtukufu wa Al Aqsa uko mikononi mwetu” ukisikika.

Maelfu ya Waisraeli pia wamefanya maandamano katika eneo hilo wakishiriki tukio la kila mwaka la kidini na kitaifa.

Maandamano hayo yanayojulikana kama “Flag March” hufanyika kuadhimisha kumbukumbu ya Israel kuteka Jerusalem Mashariki wakati wa vita vya mwaka 1967.

Mwandishi wa BBC mjini Jerusalem amesema kuwa tukio hilo mara nyingi huambatana na vurugu, misukosuko pamoja na kauli za kibaguzi dhidi ya Wapalestina wanaoishi katika maeneo hayo ya Jerusalem.

Mwaka huu, makumi ya wanaharakati wa amani kutoka Israel walijaribu kuzuia kile walichokitaja kuwa vitendo vya ukatili vinavyoambatana na maandamano hayo.

Sponsored ads

Mid 1

Mid2

Ad3