Kwa Habari za kitaifa, Kimataifa, Michezo, Burudani,Uchambuzi na matangazo. Matukio Daima Blog, Ni yetu Sote!
BILIONI 1.2 KUTUMIKA KUZUIA UCHAFUZI ZIWA TANGANYIKA

BILIONI 1.2 KUTUMIKA KUZUIA UCHAFUZI ZIWA TANGANYIKA

 

Na Fadhili Abdallah,Kigoma


WAJASILIAMALI wadogo mkoani Kigoma wanaofanya shughuli za ukusanyaji taka za plastiki na chuma chakavu zinazorejeshwa ili  kutengeneza bidhaa wanatarajia kunufaika na ruzuku ya shilingi Bilioni 1.2 zinazotolewa na Shirika la Cathoric Relief Services (CRS) ikiwa ni mradi wa kuzuia uchafuzi katika ziwa Tanganyika (VOICES).


Mratibu wa Shirika la CRS ofisi ndogo ya Kigoma, Sinyonzile Samwel akizungumza katika mkutano na wajasiliamali hao uliofanyika mjini Kigoma alisema kuwa Shirika hilo kupitia mradi VOICES limefungua dirisha la maombi kwa awamu ya pili kwa vikundi mbalimbali vinavyojishughulisha na biashara ya ununuzi na ukusanyaji wa taka za plastiki na chuma chakavu.


Samweli alisema kuwa katika madirisha haya mawili likianza la awali mwaka jana na hili lililofunguliwa Machi 25 jumla ya shilingi Bilioni 1.2 zimetengwa kwa wajasiliamali ambao maandiko yao yatakidhi vigezo kupata mkopo huo kwa wakati huu ambapo kiwango cha kiasi gani kikundi kinatapa kinatokana na andiko mradi la kikundi husika.


Mratibu huyo alisema kuwa mradi huo ulioanza mwaka 2023 umekuja kunusuru ongezeko kubwa la taka hasa za plastiki ambazo kwa kiasi kikubwa haziozi zinazoingia kwenye ziwa Tanganyika na kuleta athari kwa mazingira na kusababisha mabadiliko ya tabia nchii hivyo mrai huo kwa sehemu yake unajaribu kukabiliana na changamoto hiyo.


Akifungua mkutano wa mazungumzo ya kibiashara uliohusisha wajasiliamali wadogo, taasisi za fedha na wadau mbalimbali ulioandaliwa na Shirika lisilo la kiserikali la Cathoric Relief Services (CRS) kwa ufadhili wa jumuia ya Ulaya Katibu Tawala wa mkoa Kigoma,Hassan Rugwa alisema kuwa utekelezaji wa mradi huo ni moja ya mipango ya serikali katika kulinda uchafuzi wa ziwa Tanganyika. 


Katika hotuba iliyotolewa kwa niaba yake na Katibu Tawala Msaidizi huduma za elimu katika ofisi ya Mkuu wa mkoa Kigoma, Pauline Ndigeze alisema kuwa ujasiliamali wa kuokota taka za plastiki kwa sasa ni biashara kubwa na imetengeneza ajira nyingi kwa vijana hivyo ameomba vijana Zaidi kujitokeza kwani kuna miradi mingi ya kulinda na kuhifadhi ziwa Tanganyika ambayo inahusisha uzuiaji taka kuingia ziwani hivyo vijana wengi wanaweza kupata fursa kubwa kuanzisha shughuli za uchumi rejeshi.


Kwa upande wake Mjasiliamali anayekusanya taka za Plastiki kutoka mji mdogo wa Nguruka wilaya ya Uvinza mkoani Kigoma alisema kuwa biashara ya kukusanya taka za Plastiki inalipa lakini kwanza kuwa na mtaji wa kutosha wa kununua chupa zilizotumika kutoka kwa wakusanyaji wadogo ili kuwa na mzigo wa kutosha kuweza kuuza kwenye viwanda vinavyotengeneza bidhaa za plastiki kwenye mikoa ya Dar es Salaam na Mwanza.

Sponsored ads

Mid 1

Mid2

Ad3