*MKURUGENZI BAHI AMKABIDHI BI. MASEKA MILIONI 2.6 KUFUATIA MAAGIZO YA WAZIRI MKUU*
Sep 5, 2026
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Bahi Bi. Albina William Mtumbuka, leo amemkabidhi Bi. Agnetha Maseka kiasi cha Shilingi milioni 2.6
Fedha hizo ni malipo ya madai ya huduma ya chakula pamoja na usafirishaji wa mizigo. Malipo hayo yanakuja baada ya Waziri Mkuu, Dkt. Mwigulu Nchemba, kutoa agizo la kulipwa papo hapo leo tarehe 5 Septemba, 2026 wakati wa Mkutano wake wa hadhara.


