TAKRIBANI WATOTO 14 WAMETEKETEA WAKIWA HOSPITALINI, NCHINI PAKISTAN
Aug 26, 2026
Takriban watoto wachanga 14 wamefariki baada ya moto kuteketeza wodi ya watoto katika hospitali moja mjini Islamabad, nchini Pakistan.
Moto huo unasemekana kusababishwa na hitalafu ya mfumo wa kiyoyozi.
Moto huo ulianza mapema leo asubuhi katika Taasisi ya Sayansi za Tiba ya Pakistan (PIMS), kwenye ghorofa la tatu lenye wodi ya mama na mtoto.
Tukio hilo ni miongoni mwa matukio mabaya zaidi ya moto kuwahi kutokea katika hospitali nchini Pakistan.
Kulikuwa na watoto wachanga 16 katika wodi hiyo wakati moto huo ulipozuka, mmoja aliokolewa.
Waziri Mkuu wa Pakistan, Shehbaz Sharif, amezitaka mamlaka husika kufanya uchunguzi wa haraka kuhusu tukio hilo.
“Wahusika wanapaswa kutambuliwa na hatua kali zaidi zichukuliwe,”