Kwa Habari za kitaifa, Kimataifa, Michezo, Burudani,Uchambuzi na matangazo. Matukio Daima Blog, Ni yetu Sote!
POLISI YAWATAKA WANANCHI KUWAJUA JIRANI ZAO

POLISI YAWATAKA WANANCHI KUWAJUA JIRANI ZAO

 Na Lilian Kasenene, Morogoro

maipacarusha20@gmail.com

JESHI la Polisi nchini limewataka wananchi kuwajua majirani zao na wageni wanaoingia katika maeneo yao ili kulinda amani na kukomesha uhalifu. 

Kamishna wa Polisi Jamii Tanzania, CP Alex Mukama, alisema hayo katika Tamasha la Nne la Utamaduni wa Tanzania linaloendelea mkoani Morogoro.

Alisema ni muhimu kila mwananchi kumtambua jirani yake na kufahamu wageni wanaoingia katika eneo lake, pamoja na kujua iwapo wapo nchini kihalali.

“Huku kuna Polisi Jamii, Uhamiaji wana kaulimbiu ya ‘Mjue Jirani’ na sisi ni nyumba moja. Lengo ni kuhakikisha kila Mtanzania anakuwa mlinzi wa amani popote alipo,” alisema CP Mukama.

Alisema wakati Jeshi hilo likiadhimisha miaka 20 tangu kuanzishwa kwa Polisi Jamii, limeendelea kutoa elimu kwa umma kuhusu umuhimu wa kutunza amani, kupinga vitendo vya uhalifu na kufanya shughuli za kuinua uchumi.

“Hatuwakatai wageni, lakini ni lazima tujue kama wageni hao wako nchini kwa kufuata sheria na taratibu na kama shughuli zao zinatambulika,” alisema CP Mukama.

CP Mukama alilitaka Jeshi la Polisi kuendelea kutoa elimu kwa wananchi na kushirikiana na Polisi Jamii katika kukomesha uhalifu kwenye maeneo yao na taifa kwa ujumla.

Aliongeza kuwa Jeshi hilo pia linaendelea kutoa elimu kuhusu madhara ya biashara na matumizi ya dawa za kulevya kwa lengo la kulinda jamii, hasa vijana.

TAMASHA LA UTAMADUNI


Wakizungumza katika tamasha hilo, baadhi ya washiriki walilishukuru Serikali kwa kuanzisha tamasha hilo, wakisema linasaidia kuikumbusha jamii umuhimu wa kulinda na kutunza utamaduni wa Tanzania.

“Mikusanyiko ya aina hii ni muhimu ili kuwaonyesha vijana umuhimu wa kulinda mila na tamaduni za jamii zetu,” alisema Yusuphu Kilulu kutoka mkoani 


Alisema kizazi cha sasa kimeanza kupuuza matumizi ya vyakula na vinywaji vya asili kwa kuviona kuwa ni vya kizamani, huku akisisitiza umuhimu wa kurejea kwenye vyakula vya 

“Utandawazi umeathiri kizazi cha sasa. Vijana wanaiga tamaduni za kigeni wakiona za kwetu ni za kishamba, lakini hata huko wanakoiga wana tamaduni na mila ambazo wanazitunza,” alisema Kilulu.

Mwisho.

Sponsored ads

Mid 1

Mid2

Ad3