Kwa Habari za kitaifa, Kimataifa, Michezo, Burudani,Uchambuzi na matangazo. Matukio Daima Blog, Ni yetu Sote!
ASKOFU DKT MPELI  AMPA POLE MKURUGENZI MATUKIO DAIMA KWA KIFO CHA KAKA YAKE

ASKOFU DKT MPELI AMPA POLE MKURUGENZI MATUKIO DAIMA KWA KIFO CHA KAKA YAKE

 


Askofu wa kanisa la Ushinde Center Tanzania Dkt Mpeli James Mwaisumbe ametuma salamu za pole kwa mkurugenzi wa Matukio Daima Media Francis Godwin kwa kuondokea wa kaka yake mkubwa.

Askofu Dkt Mwaisumbe alisema amepokea kwa masikitiko makubwa kifo cha John na kuwa familia ya Ushindi Center ,DBL na Matukio Daima  ni ndugu na siku zote zimekuwa na ushirikiano na kuwa kifo hicho na pigo kwa Matukio Daima na kanisa la DBL na Kituo cha yatima cha DBL .

Hata hivyo alisema pindi alipopatwa na msiba wa kufiwa na baba yake mzazi marehemu Mwaisumbe Matukio Daima Media walisafiri hadi Tukuyu kushiriki mazishi pamoja na kurusha Live tukio hilo jambo ambalo ni upendo wa Agape kwa familia hizo mbili.

"Akayafuta kila chozi katika macho yao; wala mauti haitakuwapo tena; wala huzuni, wala kilio, wala maumivu hayatakuwapo tena; kwa kuwa mambo ya kwanza yamekwisha kupita."
— Ufunuo 21:4



Huku Uongozi na familia ya Matukio Daima Media ukitoa shukrani za dhati kwa Askofu Dkt. Mpeli James Mwaisumbe kwa moyo wake wa upendo, huruma na huduma ya kiroho aliyoionesha kwa kumfariji Mkurugenzi wa Matukio Daima Media, Francis Godwin, kufuatia msiba wa kufiwa na kaka yake mpendwa.

Katika kipindi hiki kigumu cha majonzi, uwepo wako, maneno yako ya faraja, maombi na ushirika wa kiroho vimekuwa chanzo kikubwa cha nguvu, tumaini na faraja kwa familia nzima. 

Umeonyesha kwa vitendo kuwa mchungaji wa kweli anayesimama na waumini na jamii katika nyakati za furaha na huzuni.

Tunamshukuru Mungu kwa kukujalia hekima, moyo wa upendo na utumishi wenye kugusa maisha ya watu wengi.

 Tunatambua kuwa huduma yako ya kuwafariji wenye huzuni ni sehemu ya wito wa Mungu wa kuponya mioyo iliyovunjika na kuwatia watu nguvu ya kuendelea mbele kwa imani.

Neno la Mungu linasema katika 2 Wakorintho 1:3–4: “Na ahimidiwe Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo, Baba wa rehema na Mungu wa faraja yote; atufarijie katika dhiki zetu zote, ili na sisi tupate kuwafariji walio katika dhiki yo yote, kwa faraja ile ile ambayo sisi wenyewe tunafarijiwa na Mungu.”

Kwa niaba ya Francis Godwin, familia yake na timu nzima ya Matukio Daima Media, tunasema asante sana kwa upendo wako wa dhati, maombi na faraja yako. Tunamuomba Mwenyezi Mungu aendelee kukulinda, akupe afya njema, akuongezee neema na kuibariki huduma yako ili uendelee kuwa chombo cha amani, tumaini na baraka kwa watu wengi.

Mungu akubariki sana, Askofu Dkt. Mpeli James Mwaisumbe.

Sponsored ads

Mid 1

Mid2

Ad3