Kwa Habari za kitaifa, Kimataifa, Michezo, Burudani,Uchambuzi na matangazo. Matukio Daima Blog, Ni yetu Sote!
MAREKANI YAONDOA VIKWAZO DHIDI YA MAFUTA YA URUSI KWA MARA YA PILI

MAREKANI YAONDOA VIKWAZO DHIDI YA MAFUTA YA URUSI KWA MARA YA PILI

 

Marekani imetangaza kuongeza muda wa kuondolewa vikwazo kwa mafuta ya Urusi yaliyoko baharini kwa siku 30, ili kuzisaidia mataifa yaliyo katika hatari ya kukosa mafuta.

Waziri wa Fedha wa Marekani, Scott Bessent, alisema “tumetoa leseni ya muda kusaidia mataifa yaliyoko kwenye hatari zaidi kununua mafuta ya Urusi, na leseni hii itasaidia kuimarisha bei ya mafuta ghafi kwenye soko la kimataifa” Kiongozi huyo alichapisha kwenye mtandao wa X.

Bessent, ambaye awali alisema kuwa hakukuwa na mpango wa kuongeza tena msamaha huo wa vikwazo vya mafuta ya Urusi, alidai kuwa hatua hiyo itasaidia kuhakikisha mataifa yenye uhitaji, yanapata mafuta.

Hii ni mara ya pili kwa wizara ya fedha ya Marekani kuondoa vikwazo dhidi ya mafuta ya Urusi.

Sponsored ads

Mid 1

Mid2

Ad3