Kwa Habari za kitaifa, Kimataifa, Michezo, Burudani,Uchambuzi na matangazo. Matukio Daima Blog, Ni yetu Sote!
SABABU ZA VIJANA KUTUMIA VILEVI

SABABU ZA VIJANA KUTUMIA VILEVI

 

NA EASTER KAMETA (UoI)

MATUKIO DAIMA 

Baadhi ya vijana mkoani Iringa waeleza sababu zinazopelekea baadhi ya vijana  kutumia vinywaji vyenye vilevi huku wakitaja kuwa ni njia moja wapo ya kupunguza msongo wa mawazo.


Upendo sapari ambaye  ni mkazi wa semtema amezungumza na Matukio Daima  na kusema kuwa vijana wengi hutumia vilevi  kutokana na msongo wa mawazo huku akitaja baadhi ya sababu ambazo zinawafanya vijana wengi kuwa na hali hii na kudaikuwa ukosefu wa ajira ni chanzo.

"Msongo wa mawazo hufanya vijana wengi Kujiingiza katika ulevi hali hii hutokana na changamoto kama ukosefu wa ajira, matatizo ya familia, au shinikizo la maisha hivyo hupelekea baadhi yao kuanza matumizi ya vilevi huku wakidhani kuwa ni  njia sahihi ya kutuliza au kukimbia matatizo."

Aidha kwa upande wake Patson Benard ameeleza kuwa baadhi ya vijana hufuata ushawishi wa marafiki huku akitaja kuwa   vijana wengine wanapoona rafiki zao wanatumia vilevi hivyo hufanya na wao kutamani kufanya majaribio ya kutumia vilevi .

"Ushawishi wa marafiki Kama kundi  la marafiki wanao tumia vilevi, ni rahisi kwa kijana kujiunga ili ajisikie anakubalika au asiwe tofauti na wengine pia udadisi na majaribio kwa baadhi ya vijana huanza kwa kutaka tu kujaribu kujua vilevi vina athari gani pale wanapo ona vijana wenzao wanavitumia ambao ni kundi lika nao hivyo  hupelekea na wao kuiga na kuanza  matumizi ya vilevi."

Vilevile Diana Reonard mkazi wa kihesa  ameeleza kuwa  vijana wengi hawana elimu juu ya madhara yanayotokana na utumiaji wa vinywaji vyenye vilevi pia ametaja kuwa wengine hutumia vilevi kwasababu ya matatizo ya akili na kihisia wakidai  ni njia ya kujifariji ambapo si sahihi.

" Vijana wengi hawana elimu ya kutosha  kuhusu matumizi ya vilevi na wengine hawajui madhara ya muda mrefu ya vilevi, hivyo huanza bila kuelewa hatari  na wengine hutumia vilevi katika matatizo ya kihisia au afya ya akili katika hali kama huzuni, upweke, au hata magonjwa ya akili vijana wengi huamini matumizi ya vilevi kama njia ya kujifariji."

Pia shadrack Jumanne ametaja kuwa upatikanaji rahisi  wa vilevi katika mazingira yanayo zunguka vijana ni chachu ya wao kufanya matumizi  hayo pia ametaja kuwa baadhi ya vijana huiga mifano mibaya kutoka kwa wanaowazunguka na wengine katika mitandao ya kijamiii.

" Upatikanaji rahisi wa vilevi Kama pombe au dawa za kulevya katika mazingira wanayo patiakana vijana matumizi ya vilevi huwa ni rahisi kuanza pia kuiga mifano mibaya kutoka kwa watu wanaowazunguka au wanaowaona kwenye mitandao ya kijamii wanaotumia vilevi  na hupelekea vijana wanaweza kuona ni jambo la kawaida."

Sponsored ads

Mid 1

Mid2

Ad3