Kwa Habari za kitaifa, Kimataifa, Michezo, Burudani,Uchambuzi na matangazo. Matukio Daima Blog, Ni yetu Sote!
HALI YA BIASHARA YA USAFIRI WA DALADALA MKOANI IRINGA

HALI YA BIASHARA YA USAFIRI WA DALADALA MKOANI IRINGA

Na Catherin Kilwale (UoI) Matukio Daima Media 

Baadhi ya madereva daladala  Manispaa ya Iringa mjini,Wameeleza hali halisi ya biashara ya usafiri wa daladala kutokana na kupanda kwa bei ya mafuta  msimu huu,na kupelekea kupanda kwa nauli kwa baadhi ya vyombo vya usafiri.

Kwa upande wake  makamu mwenyekiti wa Umoja wa  madereva daladala  Manispaa ya Iringa,Salimu  Ngoda  amesema kuwa hali ya biashara ya usafiri kwa daladala  sasahivi wateja  niwengi kutokana na  kutokupanda  kwa bei ya nauli, kwani bei yetu sisi ni elekezi kutoka Mamlaka husika.


Licha ya hivyo sisi kama madereva daladala  hatujapandisha nauli ili kuwa rahisishia abilia wetu kusafiri kwa urahisi, pia halisi hii inasababisha daladala kuonekana chache kutokana na uwingi wa abilia  ambao wana kwepa kupanda bajaji kutokana na  kupanda kwa bei ya nauli.

"Tunaiomba Serikali   yetu itusaidie kulinda daladala ambazo zinachukuwa bei rafiki kwa abili, ili hata mafuta  yakipanda zaidi tuweze kuwa saidia abiria kusafiri  maana bila hvyo abilia watashindwa kusafili kabisa kuelekea katika shughuli zao".

Huku Philipo Nyalusi   mkazi wa Iringa,ambaye ni abilia amesema kuwa kutokana na kupanda kwa bei ya mafuta kumepelekea hadi nauli kupanda, kwani  tulizoea zamani nauli ya bajaji ni mia saba (700) lakini sasahivi  ni elfu moja(1000)  hali hii inakusanya kutumia  bajeti kubwa kwa siku.

"Sisi kama abilia tunaomba serikali itusaidie kutoa bei elekezi za usafiri ili kuweka usawa, kwani tukiangalia wanaoumia sana ni wanafunzi wanashindwa kufika shule kutokana na bei ilivyo panda  kwa kasi kikubwa upande wa bajaji".

Nae Neema Godfrey ambaye ni mwanafunzi  amesema kuwa kwa sasa hivi sisi wanafunzi tunapata changamoto  kubwa ya usafiri tunapoelekea shuleni kutokana na kupanda kwa bei ya nauli.

"Kutokana na bei ya usafiri  inayotembea sasa, inapelekea  wanafunzi kushindwa kufika shule  na kusababisha kukosa   kuhudhuria masomo na kurudi nyuma  katika  maendeleo  ya kielimu, kutokana na hali tunazo kutananazo barabarani".

Tunaomba  serikali itusaidie kutoa  bei   elekezi ya mafuta na naulii ili kuwasaidia madereva na abilia kujua bei halisi na kuweka sheria  kali kwa  watakao  kiuka sheria  zilizowekwa.

Sponsored ads

Mid 1

Mid2

Ad3