Kwa Habari za kitaifa, Kimataifa, Michezo, Burudani,Uchambuzi na matangazo. Matukio Daima Blog, Ni yetu Sote!
DKT TUMAIN MSOWOYA AWATIA MOYO WANAWAKE KUTOKATA TAMAA

DKT TUMAIN MSOWOYA AWATIA MOYO WANAWAKE KUTOKATA TAMAA


Mwanahabari na Mtumishi wa Mungu na Mwimbaji wa Nyimbo za Injili, Dk Tumaini Msowoya ameshiriki na kutoa darasa katika kongamano la Wanawake wa Kikristo lililofanyika katika ukumbi wa Royal Palm, Mjini Iringa. 


Kongamano hilo lililo andaliwa na Mchungaji Winnie Msami, kiongozi wa Kanisa la Living Water liliwakusanya mamia ya wanawake kwa lengo la kujifunza masuala mbalimbali kuhusu maisha na baadae maombi. 

Msowoya aliwataka wanawake wasikubali kukata tamaa badala yake wakubali kujifunza mambo mapya kila siku. 

"Elimu siku hizi ni nyingi, sio kama zamani. Tusiache kujifunza na marufuku kukata tamaa mpaka mkatisha tamaa afe. We can," amesema.

Sponsored ads

Mid 1

Mid2

Ad3