TRUMP ASEMA MAREKANI ITAONDOKA IRAN NDANI YA 'WIKI MBILI AU TATU' IWE 'KUNA MAKUBALIANO AU LAAH
Rais Donald Trump amewaambia waandishi wa habari kwamba Marekani "itaondoka[Iran] hivi karibuni" na hatua za kijeshi za nchi hiyo zitakomeshwa ndani ya "wiki mbili au tatu"
Anasema Marekani imefikia malengo iliyojiwekea kabla ya kuanza kwa mashambulizi ya anga dhidi ya Iran mwezi uliyopita kwa ushirikiano na Israel.
Ameongeza kuwa lengo la kuizuia Iran kuwa na uwezo wa kuunda silaha za nyuklia limefikiwa na sasa Marekani "inamaliza kazi"
Trump pia anasema Marekani sasa inatawala anga la Iran na pia imepata mabadiliko ya utawala kufuatia mauaji ya viongozi wakuu wa kisiasa na kijeshi.
Aliwataja viongozi hao wapya mjini Tehran kama "walio na misimamo mikali" na "waadilifu zaidi" ikilinganishwa na watangulizi wao.
Trump pia anasema viongozi wa Iran "wanaomba kufanya makubaliano" na Marekani ili kumaliza vita, madai ambayo hapo awali yalipingwa na Iran.
Anaongeza kuwa vita vinaweza kumalizika bila makubaliano kati ya pande hizo mbili.
Kuhusu athari za vita hasa kupanda kwa bei ya mafuta, rais Trump anasema bei itashuka mara tu Marekani itakapomaliza hatua zake za kijeshi.