Kwa Habari za kitaifa, Kimataifa, Michezo, Burudani,Uchambuzi na matangazo. Matukio Daima Blog, Ni yetu Sote!
TUANZEBE AIREJESHA DR CONGO KWENYE KOMBE LA DUNIA BAADA YA MIAKA 52

TUANZEBE AIREJESHA DR CONGO KWENYE KOMBE LA DUNIA BAADA YA MIAKA 52

 

Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo imejihakikishia tiketi ya Kombe la Dunia kwa mara ya kwanza katika kipindi cha miaka 52, baada ya Axel Tuanzebe kufunga bao la dakika za nyongeza lililowapa ushindi wa 1-0 dhidi ya Jamaica katika fainali ya mchujo ya bara, iliyopigwa kwenye Uwanja wa Guadalajara nchini Mexico.

Wakati wa maandalizi ya mechi hiyo, Tuanzebe aliliambia BBC kuwa mchezo huo ulikuwa mkubwa zaidi katika maisha yake ya soka.

Beki huyo wa zamani wa timu ya taifa ya Uingereza, ambaye alizaliwa Bunia, mji uliokumbwa na machafuko ya muda mrefu mashariki mwa DR Congo, sasa ameandika historia mpya kwa taifa hilo.

Licha ya mshambuliaji wa Leopards, Cédric Bakambu, kukosa mabao mawili yaliyokataliwa kwa kuotea katika muda wa kawaida, haikushangaza kwamba pambano hilo lililokuwa na ushindani mkubwa lililazimika kuamuliwa katika dakika 30 za nyongeza.

Ndipo Tuanzebe alipokuwa mahali sahihi kwa wakati sahihi, akitumia mwili wake kuunganisha mpira wa kona uliopigwa na Brian Cipenga na kuutumbukiza wavuni.

Shangwe zilisitishwa kwa muda huku waamuzi wakipitia tukio hilo kwa VAR kufuatia tuhuma za mpira wa mkono, lakini hatimaye ilithibitishwa kuwa hakukuwa na kosa, na bao hilo likasalia halali.

Kwa upande mwingine, Jamaica waliokuwa wakisaka kufuzu kwa Kombe la Dunia kwa mara ya pili tangu waliposhiriki mwaka 1998 nchini Ufaransa walishindwa kuunda nafasi za maana za kusawazisha bao na badala yake, ni DR Congo ambao sasa watajiunga na Kundi K katika michuano hiyo iliyopanuliwa ya timu 48.

DR Congo wataanza dhidi ya Ureno mjini Houston tarehe 17 Juni, kabla ya kukutana na Colombia na Uzbekistan.

Sponsored ads

Mid 1

Mid2

Ad3