Kwa Habari za kitaifa, Kimataifa, Michezo, Burudani,Uchambuzi na matangazo. Matukio Daima Blog, Ni yetu Sote!
HALI HALISI YA BIASHARA YA MIHOGO MSIMU HUU WA MFUNGO

HALI HALISI YA BIASHARA YA MIHOGO MSIMU HUU WA MFUNGO

 

Na Catherin Kilwale  (UoI) Matukio Daima Media.

Wafanyabiashara  wa mihogo  waliopo katika soko kuu la Mkoa wa Iringa wameeleza hali halisi ya biashara hiyo msimuhuu wa mfungo wa ramadhani na kwaresma,pia wamesema kuwa upatikanaji wa zao hilo ni mdogo kutokana na wahitaji  ni wengi sana.

Wakizungumza na Matukio Daima Media, baadhi ya wafanyabiashara hao  wameeleza kuwa msimu huu wa mfungo  bei ya mihogo ipo juu, tofauti na misimu mingine.

Mfanayabiashara Ibrahim azary, alisema kupanda kwa bei ya mihogo msimu huu wa mfungo unatokana na baadhi ya miundombinu  ya barabara ni mbovu  kutoka kwa wakulima hadi kutufikia sokoni.

"Bei ya mihogo imekuwa  juu kutokana na  sisi wafanyabiashara  tukifika mashambani inakozalishawa  tunakutana na bei ipo juu, kutokana na  hali  ya hewa ya msimu huu ni mvua hupelekea upatikanaji mchacha wa zao hili".

Kwaupande wake  mafanayabiashara Hadija Rajab amesema kuwa  msimu huu wa mfungo wa Ramadhani  na kwaresma  hali ya biashara  ya mihogo ipo juu kutokana na watumiaji ni wengi,pia  mihogo hutumika kuanda futari kwa watu walio funga.

"Msimu huu wa mfungo tunajumua mihogo kwa bei kubwa kutokana na mfungo kwani  gunia moja tunanunua kwa 150,000 ambapo msimu uliopita tulikuwa tunanunua kwa 135,000 ambayo hupelekea na sisi wauzaji kupandisha bei  ya mihogo".

Huku Paulina Mligo,ambeye ni mununizi wa mihogo amesema kuwa   zao hili  linnapatika kwa shida sana pia bei imepanda  kutokana na mfungo, watu wengi wanaitumia mihogo kwajili ya kuandaa chakula mda wa kufungua.

"Kabla ya mfungo kuanza  bei ya  mihogo ilikuwa ya kawaida lakini  kufikia msimu wa mfungo bei ya mihogo imekuwa kubwa mbapo fungu moja unaumwa kwa 1000 ambapo sahzi fungu la elfu moja hakuna inaanzia shilingi 2000,  bei hii inatu athiri sisi wanunuzi".

Hata hivyo wafanyabiashara hao wameiomba serikali  iwaasaidia kuboresha miundo mbinu ya barabara  kutoka vijijini kuja mjini ili kuwasaidia katika usafirishaji wa  mazao kutoka kwa wakulima  hadi kufika sokoni,ilikupunguza gharma kubwa ya usafirishaji na kulinda kipato chao msimu huu wa mfungo kutokana na hali iliyopo.

Sponsored ads

Mid 1

Mid2

Ad3