Kwa Habari za kitaifa, Kimataifa, Michezo, Burudani,Uchambuzi na matangazo. Matukio Daima Blog, Ni yetu Sote!
 UBORA WA SHULE ZA ST DOMINIC SAVIO ,WAPONGEZWA NA WAZAZI

UBORA WA SHULE ZA ST DOMINIC SAVIO ,WAPONGEZWA NA WAZAZI


NA MATUKIO DAIMA MEDIA

IRINGA

WAZAZI wa wanafunzi wanaosoma katika Shule za St. Dominic Savio mkoani Iringa wamepongeza uongozi wa shule hizo kwa kuandaa ziara za kielimu zinazowawezesha wanafunzi kujifunza kwa vitendo na kuongeza uelewa nje ya mazingira ya darasa.

Wazazi hao wamesema ziara hizo ni sehemu muhimu ya elimu, kwa kuwa zinawapa wanafunzi fursa ya kujionea na kuelewa kwa vitendo mambo wanayofundishwa darasani, ikiwemo historia, utamaduni na uhifadhi wa mazingira.


Akizungumza kwa niaba ya wazazi wengine, Shukuru Mpelele, mkazi wa Zanzibar, amepongeza juhudi za shule hiyo za kuwapeleka wanafunzi kutembelea maeneo mbalimbali nchini kwa lengo la kuongeza maarifa na ujuzi.

“Wazazi tuna wajibu wa kuendelea kushirikiana na walimu katika kugharamia na kuunga mkono programu za kielimu kama hizi, kwa kuwa manufaa yake kwa watoto ni makubwa na yanaweza kuwasaidia katika maisha yao ya baadaye,” alisema Shukuru.

Alisema fursa hizo zikienziwa na kuendelea kutolewa, wanafunzi wengi zaidi wataweza kujifunza mambo mbalimbali yanayoongeza maarifa na kuwaandaa kukabiliana na changamoto za maisha ya baadaye.

Aidha, Shukuru ameipongeza St. Dominic Savio kwa kuweka mazingira rafiki ya kujifunzia, kusimamia nidhamu na kuwa na walimu wanaowasimamia wanafunzi kwa karibu, akisema mambo hayo yanachangia kwa kiasi kikubwa wanafunzi kufanya vizuri kitaaluma.


Ziara hiyo imewashirikisha jumla ya wanafunzi 117 pamoja na walimu saba kutoka Shule ya St. Dominic Savio ya mkoani Iringa, ambao wameelekea Zanzibar kwa ziara ya kielimu yenye lengo la kuwapa wanafunzi fursa ya kujifunza kwa vitendo.

Wakati wa ziara hiyo, wanafunzi wanatarajiwa kutembelea maeneo mbalimbali yenye umuhimu wa kihistoria, kiutamaduni na kimazingira, huku wakipata fursa ya kujifunza moja kwa moja kutoka katika mazingira wanayoyatembelea.TAZAMA MAHOJIANO YOTE BOFYA LINK HII

Akizungumza na Matukio Daima, Mratibu wa Shule za St. Dominic, Mussa Myula, alisema ziara hiyo imehusisha makundi ya wanafunzi yanayoongozwa na walimu wao katika maeneo mbalimbali yaliyopangwa kwa ajili ya kujifunza.

Myula alisema miongoni mwa maeneo yatakayotembelewa ni misitu ya Zanzibar, ambapo wanafunzi watapata fursa ya kujifunza kuhusu mazingira, uhifadhi wa misitu na umuhimu wa rasilimali hizo katika maisha ya jamii.

“Ziara hii pia inalenga kuwafanya wanafunzi wajifunze historia ya Zanzibar kwa kujionea wenyewe maeneo mbalimbali ambayo wamekuwa wakiyasoma katika vitabu na masomo ya darasani,” alisema.

Alisema elimu ya darasani pekee haitoshi, hivyo wanafunzi wanapopewa nafasi ya kutembelea maeneo wanayojifunza, huwa rahisi kuelewa zaidi kile wanachofundishwa na kupata maarifa kupitia uzoefu wa moja kwa moja.


Kwa mujibu wa Myula, wanafunzi hao pia wanatarajiwa kukutana na viongozi pamoja na wawakilishi wa makundi mbalimbali ya vijana Zanzibar, hatua ambayo itawapa fursa ya kujifunza namna vijana wanavyoshiriki katika shughuli za kijamii na maendeleo katika maeneo yao.

“Lengo kubwa la Shule ya St. Dominic katika kuandaa ziara kama hizi ni kuwajengea wanafunzi uwezo wa kujifunza mazingira mapya, kufahamu historia na tamaduni za maeneo mbalimbali, pamoja na kupata ujuzi ambao unaweza kuwasaidia katika maisha yao ya baadaye,” alisema Myula.

Aliongeza kuwa shule itaendelea kuwapa wanafunzi fursa za kutembelea maeneo mbalimbali ndani na nje ya Tanzania, akisisitiza kuwa ziara za kielimu ni sehemu muhimu ya kuwasaidia watoto kupanua uelewa, kujifunza kwa vitendo na kutambua fursa mbalimbali zilizopo katika jamii.

KUJIUNGA NA SHULE ZETU TAZAMA HABA CHINI ⬇️⬇️


TANGAZO LA ST DOMINIC BOFYA HAPA

Sponsored ads

Mid 1

Mid2

Ad3