Kwa Habari za kitaifa, Kimataifa, Michezo, Burudani,Uchambuzi na matangazo. Matukio Daima Blog, Ni yetu Sote!
TRUMP ASEMA ITAKUWA 'KOSA KUBWA' INFANTINO AKIONDOLEWA

TRUMP ASEMA ITAKUWA 'KOSA KUBWA' INFANTINO AKIONDOLEWA

 

Rais wa Marekani Donald Trump amesema itakuwa kosa kubwa sana kumuondoa Gianni Infantino katika nafasi yake ya urais wa Shirikisho la Soka Duniani, FIFA.

Kauli ya Trump imekuja baada ya UEFA, Concacaf na Shirikisho la Soka la Asia, AFC, kumshutumu Infantino kwa kuvunja uaminifu kupitia pendekezo lake lililofutwa la uekezaji linalojulikana kama Fifa Forward Enterprise, FFE.

Pendekezo hilo lililenga kuunda kampuni mpya ya kusimamia haki za kibiashara na mauzo ya tiketi za mashindano yote ya FIFA, yakiwemo Kombe la Dunia, huku asilimia 21 ya kampuni hiyo ikiuzwa kwa kampuni binafsi ya uwekezaji.

Trump amesema FIFA itakuwa inafanya kosa kubwa ikiwa itafikiria kumwondoa Infantino.

“FIFA itakuwa inafanya kosa baya sana ikiwa, kwa sababu yoyote ile, itafikiria hata kumwondoa Rais Gianni Infantino,” Trump aliandika kwenye mitandao ya kijamii.

“Yeye ni mzuri sana, kwani hivi karibuni ameongoza Kombe la Dunia lenye mafanikio makubwa zaidi kuwahi kufanyika, mara nne zaidi. Ikiwa ataondoka, halitawahi kuwa na mafanikio au faida kubwa kama hiyo tena.”

Kombe la Dunia la mwaka 2026 liliandaliwa kwa pamoja na Marekani, Canada na Mexico msimu huu wa kiangazi, huku Hispania ikitwaa ubingwa baada ya kuifunga Argentina katika fainali.

Alipozungumzia kwa mara ya kwanza pendekezo la FFE tarehe 31 Julai, Trump alisema hajawahi kuzungumza na Infantino kuhusu mipango hiyo.

Thrive Eternal ilitarajiwa kuongoza kundi la wawekezaji lililopendekezwa kwa ajili ya FFE.

Thrive ni kampuni ya Marekani ya uwekezaji wa mitaji iliyoanzishwa na Joshua Kushner, ambaye ni kaka wa Jared, mkwe wa Trump.

Trump na Infantino wana uhusiano wa karibu.

Infantino alimtuza Trump Tuzo ya kwanza ya Amani ya FIFA mwezi Desemba 2025.

Sponsored ads

Mid 1

Mid2

Ad3