Kwa Habari za kitaifa, Kimataifa, Michezo, Burudani,Uchambuzi na matangazo. Matukio Daima Blog, Ni yetu Sote!
KINGU: NDEJEMBI NI KIJANA MZALENDO, MCHAPAKAZI

KINGU: NDEJEMBI NI KIJANA MZALENDO, MCHAPAKAZI

 

Mbunge wa Ikungi Magharibi, Elibariki Kingu amemmwagia sifa Makamu wa Rais mteule, Deogratius Ndejembi akisema ni kijana mchapakazi, mwenye uzalendo ndani yake na anayeling’arisha Taifa.

Kingu ameyasema hayo leo Agosti 28, 2026 jijini Dodoma wakati akichangia hoja ya kumthibitisha ndejembi kwenye nafasi ya Makamu wa Rais, iliyotolewa na Waziri Mkuu, Dk Mwigulu Nchemba.

Amesema Taifa limepata kijana mwenye kaliba ya unyeyekevu na kujishusha kwa kila mtu na nidhamu katika kazi anazofanya kila siku.

“Ndejembi ni kijana mchapakazi mwenye commitment ya uzalendo ndani yake. Wakati dunia inapita kwenye misukosuko ya kupanda kwa bei ya mafuta, ni kijana huyu Ndejembi aliisimamia Serikali kuhakikisha shirika letu la TPDC (Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania) linapata uhakika wa kupata mafuta kwa kipindi chote ambacho dunia inapita katika misukosuko.

“Ni kwa uzalendo huo wa kijana huyu, ameweza kuling’arisha taifa katika medani za kimataifa. Leo anapokuwa nje ya nchi tunaona uwakilishi wake na utulivu wake namna anavyoliwakilisha taifa letu,” amesema Kingu.

Sponsored ads

Mid 1

Mid2

Ad3