Kwa Habari za kitaifa, Kimataifa, Michezo, Burudani,Uchambuzi na matangazo. Matukio Daima Blog, Ni yetu Sote!
BEI YA MAFUTA DUNIANI YAPANDA BAADA YA MAREKANI NA IRAN KUZIDISHA MASHAMBULIZI

BEI YA MAFUTA DUNIANI YAPANDA BAADA YA MAREKANI NA IRAN KUZIDISHA MASHAMBULIZI

 

Bei ya mafuta katika soko la dunia imepanda kwa zaidi ya asilimia nne kufuatia hatua ya Marekani kuanzisha mashambulizi mapya dhidi ya Iran na Tehran kujibu kwa mashambulizi ya kulipiza kisasi.

Mafuta ghafi aina ya Brent yalipanda kwa asilimia nne na kufikia dola 79.11 kwa pipa, huku mafuta ghafi ya Marekani aina ya West Texas Intermediate (WTI) nayo yakiongezeka kwa asilimia nne na kufikia dola 74.36 kwa pipa, kwa mujibu wa Reuters.

Kupanda kwa bei hizo kunafuatia wasiwasi kuhusu usalama wa usafirishaji wa mafuta katika eneo la Ghuba, ambalo ni moja ya njia muhimu zaidi za biashara ya nishati duniani.

Sponsored ads

Mid 1

Mid2

Ad3