WANANDOA WA UINGEREZA WALIOFUNGWA IRAN WAANZA KUSUSIA KULA GEREZANI
May 20, 2026
Familia ya wanandoa wa Uingereza waliofungwa nchini Iran baada ya kushutumiwa kwa ujasusi imesema wawili hao wameanza kususia kula.
Lindsay Foreman na Craig Foreman walikamatwa walipokuwa wakivuka Iran kwa pikipiki mnamo Januari 2025, na baadaye walihukumiwa kifungo cha miaka kumi gerezani.
Wakati huo huo, raia wa Iran mwenye ukaazi wa kudumu nchini Marekani ameachiwa huru na kurejea Marekani baada ya kuzuiliwa kwa miaka kumi nchini Iran.
Shahab Dalili alikuwa ameshtakiwa kwa kushirikiana na serikali hasimu.