TRUMP: CHINA YATAKA MLANGO WA HORMUZ UBAKI WAZI
May 14, 2026
Rais wa Marekani Donald Trump amesema kuwa China inataka Mlango wa bahari wa Hormuz ubaki wazi, akieleza kuwa hatua hiyo ni muhimu kwa usafirishaji wa mafuta.
Aidha amesema China inanunua kiasi kikubwa cha mafuta kupitia eneo hilo, na hivyo inapendelea shughuli hizo ziendelee bila vikwazo.
Trump ameongeza kuwa Rais wa China Xi Jinping ameonyesha utayari wa kusaidia kufanikisha makubaliano ya kuhakikisha mlango huo unabaki wazi.
“Yeyote anayenunua kiasi hicho cha mafuta ana uhusiano fulani nao, lakini alisema angependa kusaidia endapo ataweza,” Trump amesema, akisisitiza kuwa China ingependa kuona Mlango wa Hormuz ukiendelea kuwa wazi.
Pia Trump amemalizia kwa kusema Marekani na China wana mtazamo unaofanana kuhusu suala la Iran.