Kwa Habari za kitaifa, Kimataifa, Michezo, Burudani,Uchambuzi na matangazo. Matukio Daima Blog, Ni yetu Sote!
TASAC, TRCS WATOA ELIMU YA UOKOAJI ZIWA TANGANYIKA

TASAC, TRCS WATOA ELIMU YA UOKOAJI ZIWA TANGANYIKA

 

Na Fadhili Abdallah,Kigoma


Shirika la Msalaba Mwekundu Tanzania (TRCS)  kwa kushirikiana na Shirika la uwakala wa meli nchini (TASAC) wameendesha zoezi maalum la utoaji elimu ya uokoaji na usalama majini kwa wakazi wanaozunguka mwambao wa Ziwa Tanganyika mkoani Kigoma kuhusu namna ya kujikinga na ajali pamoja na hatua za kuchukua wakati wa dharura majini.


Zoezi hilo lililofanyika katika maeneo mbalimbali ya mwambao wa ziwa hilo, lililenga kutoa elimu kwa wavuvi, wasafirishaji wa abiria pamoja na wananchi wanaotumia usafiri wa majini kuhusu namna ya kujikinga na ajali pamoja na hatua za kuchukua wakati wa dharura majini.


Akizungumza wakati wa zoezi hilo Afisa Mfawidhi TASAC mkoa kigoma,Adam Mamilo TASAC alieleza kuwa elimu ya matumizi sahihi ya vifaa vya uokoaji ikiwemo maboya, jaketi za kuokoa maisha na namna ya kutoa taarifa za ni muhimu katika kupunguza vifo vinavyotokana na ajali za majini.


Kwa upande wake Mratibu wa Shirika la Msalaba Mwekundu Tanzania (TRCS) mkoa wa Kigoma,  Exavery Migarambo alisisitiza umuhimu wa jamii kuwa na uelewa wa huduma ya kwanza pamoja na mbinu za kuwaokoa waathirika wa ajali za majini kabla ya kufikishwa kwenye huduma za afya.



Mmoja wa wavuvi wanaofanya shughuli zao katika mwambao wa ziwa Tanganyika, Majundo Selemani alisema kuwa  kuwa elimu hiyo imewasaidia kuongeza uelewa kuhusu tahadhari za usalama majini, hasa kipindi cha upepo mkali na mawimbi makubwa ambayo mara nyingi husababisha ajali katika Ziwa Tanganyika.


Sponsored ads

Mid 1

Mid2

Ad3