Kwa Habari za kitaifa, Kimataifa, Michezo, Burudani,Uchambuzi na matangazo. Matukio Daima Blog, Ni yetu Sote!
 SIRRO ATAKA VIKWAZO  BIASHARA ZA KUVUKA MPAKA  VIONDOLEWE

SIRRO ATAKA VIKWAZO BIASHARA ZA KUVUKA MPAKA VIONDOLEWE

Na Fadhili Abdallah,Bujumbura

Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Balozi Simon Sirro amezitaka mamlaka za kibiashara za Tanzania na Burundi kushughulikia changamoto ya vikwazo visivyo vya kikodi ili kuimarisha Biashara baina ya mataifa hayo mawili.

Balozi Sirro ametoa wito huo akizungumza katika ufunguzi wa wa maonesho ya pamoja ya biashara baina ya Tanzania na Burundi yanayofanyika jijini Bujumbura nchini Burundi yakijumuisha wajasiliamali na wafanyabiashara kutoka mkoani Kigoma na wale wa Burundi.

Akimwakilisha Waziri wa viwanda na Bishara kufungua maonyesho hayo Mkuu huyo wa mkoa Kigoma  alisemaa kuwa pande hizo mbili zina nafasi ya kushughulikia na kuondoa changamoto hizo zisizo za kikodi kurahisisha ukuaji wa biashara.

Mkuu huyo wa mkoa kigoma alisema kuwa Tanzania na Burundi zinapaswa kushughulikia vikwazo hivyo ikiwemo taratibu za zinazochukua muda mrefu , utoaji wa maamuzi ya busara bila kuzingatia kanuni na Sheria pamoja na kuharakisha utekelezaji taratibu za biashara na wafanyabiasha wanaofanya biashara za kuvuka mpaka.

Awali Balozi wa Tanzania nchini Burundi,  Gelasius Byakanwa akizungumza katika maonesho hayo  alisema kuwa maonesho hayo yamelenga kutanua wigo wa masoko na kuwezesha wafanyabiashara wapya kuingia kwenye sekta hiyo na biashara zao kuwa zenye tija.

Kwa upande wake  Josias Bigirimana ambaye ni mfanyabiashara kutoka  jiji la Bujumbura nchini Burundi alisema kuwa  maonesho hayo ya pamoja, yamewapa fursa ya kubadilishana ujuzi na taarifa za kimasoko baina yao na wafanyabiashara wa Tanzania.

Mwisho.

Sponsored ads

Mid 1

Mid2

Ad3