PAPA LEO XIV AOMBA MSAMAHA WA KIHISTORIA KUHUSU NAFASI YA VATICAN KATIKA UTUMWA
Papa Pope Leo XIV ameomba msamaha wa kihistoria akikiri jukumu la Holy See katika kuhalalisha utumwa na kushindwa kuupinga kwa karne nyingi, akielezea rekodi hiyo ya Kanisa kama “jeraha katika kumbukumbu ya Kikristo.”
Kauli hiyo inachukuliwa kuwa moja ya hatua kali zaidi zilizowahi kuchukuliwa na Papa kuhusu kukiri moja kwa moja kuhusika kwa mamlaka za zamani za Vatican katika kuruhusu na kuendeleza utumwa wa watu wasio Wakristo katika enzi ya ukoloni.
“Kwa hili, kwa niaba ya Kanisa, naomba msamaha kwa dhati,” ameandika katika waraka wake mpana, akieleza “huzuni kubwa” kutokana na mateso yaliyowakumba watu waliokuwa watumwa.
Pia alikiri kwamba kabla ya kipindi hicho, katika Zama za Kati, taasisi za kanisa nazo zilikuwa na watumwa wake wenyewe.
Alisema Kanisa lilifikia tu “hukumu rasmi, ya moja kwa moja na ya kimataifa” dhidi ya utumwa katika karne ya 19 chini ya Papa Leo XIII, baada ya kile Papa wa sasa alichokieleza kuwa kipindi kirefu cha ukinzani katika mafundisho na utekelezaji wake.