POLISI MOROGORO, VIKUNDI VYA KARETI WAIBUA MKAKATI WA KUOKOA VIJANA WALIOKUMBWA NA DAWA ZA KULEVYA
*Na Lilian Kasenene, Morogoro*
Matukio DaimaApp
JESHI la Polisi Mkoa wa Morogoro, kupitia kitengo cha Polisi Jamii kwa kushirikiana na kikundi cha mazoezi ya kareti cha SAYDO KARATE, limeanzisha oparesheni maalum ya kuwafikia vijana wanaojihusisha na uuzaji wa dawa za kulevya aina ya bangi mitaani, kwa lengo la kuwabadilisha na kuwa sehemu ya jamii yenye tija.
Kuanzia Januari mwaka huu, vijana hao wamekuwa wakikusanywa na kupewa elimu kuhusu madhara ya dawa za kulevya pamoja na mafunzo ya stadi za maisha. Baada ya hapo, wameunganishwa katika vikundi vya ujasiriamali ili kuwapatia njia mbadala ya kujipatia kipato halali na kuachana na vitendo vya uhalifu.
Mkuu wa Polisi Jamii Mkoa wa Morogoro, ACP Samwel Kijanga, amesema kuwa mabadiliko ya kifikra, mtazamo na matendo kwa vijana hao yamechangia kwa kiasi kikubwa kupungua kwa matukio ya uhalifu katika maeneo mbalimbali ya mkoa huo.
.jpg)


