UMUHIMU WA WAUMINI KUFUNGA NA FAIDA ZAKE
NA EASTER KAMETA (UoI)
MATUKUO DAIMA
Waumini wa dini ya Kikristo na Kiislamu mkoani Iringa wahimiza juu ya suala kufunga hasa msimu huu wa kwaresma na ramadhani pia wataja baadhi ya faida atazo zipata mtu iwapo atafunga.
Akizungumza,na matukio daima Abuubakar Omarry ameeleza maana ya ramadhani ,huku akitaja baadhi ya baadhi ya matendo ambayo mtu hapaswi kuyanya mda wa funga kama vile kufanya matendo ya kiovu
"Ramadhani hii nifunga ya kumkarbia mwenyezi mungu kwa njia ya kufunga pia msimu huu wa ramadhani muumini hipaswi kufanya matendo yasiyo faa wala yasiyo mpendeza mwenyezi mungu matendo hayo kama ulevi ,wizi ,dhuruma ukifanya hivyo utakua umeenda kinyume na mwenyezi mungu pia umeharibu funga yako kama muhislam."
Isaac Abasi ameeleza maana ya kwaresma huku akitaja kuwa kupitia kwaresma watu wengi wanapata kumkaribia mungu pia ametaja kuwa kwaresma ni chachu ya watu kuwa na maadili mema.
"Msimuu huu wa kwaresma wakristo tunaufanya kama mwezi ambao unatukutanisha kati ya mwanadamu na Mungu pia kwaresma inawahimiza watu kufanya yaliyo mema kama vile kuhimiza watu kumtumaini Mungu kuwa na upendo na kudumisha amani na kudumisha maadili mema Pia kupiga vita mambo yanayo kwenda kinyume na dini kama vile uasherati ,ushirikina"
Mwanahamisi Hamisi ameeleza baadhi ya faida ambazo mtu aliye funga atazipata Huku akitaja kuwa faida hizi atazipata katika upande wa afya ya mwili na katika upande wa kiroho akitaja kuwa watu wataimarika zaidi.
"Mtu aliye funga ataimarika kiroho pia nafsi yake itakuwa ikitaja hasa mambo yaliyo mema pia katika afya ya mtu aliye funga itakuwa salama kwasababu mmeng'enyo wa chakula utakaasa ,mwili kuwa mwepesi pia ataepuka baadhi ya magonjwa kama vile homa ya matumbo, unene kupitiliza ,presha ,kisukari"
Rahma Hassan amewataka waumini wote wapate kufunga ili kuepuka baadhi ya mambo huku akishauri jamii na watu wake kwa kuwaonyesha baadhi ya mambo ambayo wanapaswa kufanya msimuu huu wa hizi funga zote mbili.
"Jamani tufunge kuanzia matendo hadi roho na nafsi zetu kwani mtu ikiwa umefunga afu unasengenya hapohujafunga weendelea kula tu pia mtu unapo funga hupaswi kufanya vitu ambavyo viko kinyume na maadili ya dini kama ulevi ambao hufanya mtu kufanya vitu vya kikatili, watu wanapaswa kuwa na lugha nzuri ya ukarimu na ushilikiano upendo kwa watu wote na dini zote ubaguzi haufai"
