Kwa Habari za kitaifa, Kimataifa, Michezo, Burudani,Uchambuzi na matangazo. Matukio Daima Blog, Ni yetu Sote!
ADHARA YA VIJANA KUTUMIA POMBE WAKIWA NA UMRI MDGO

ADHARA YA VIJANA KUTUMIA POMBE WAKIWA NA UMRI MDGO

 


Na Catherin  Kilwale  (UoI)Matukio Daima Media.

Mganga Mkuu wa Zahanati ya Ngome Kata ya Kihesa Mkoani Iringa, John  Mlunguza  ameleza kuwa matumizi ya pombe kupita kiasi  kwa baadhi ya vijana yamekuwa changamoto katika jamii,kwanii yanapelekea  vijana wengi  kuathirika kiafya.

Amesema kuwa vijana wengi wa kizazi hichi wanatumia  pombe kali pasipo kujua zinaleta athari  gani katika mwili,pia wengine husema kuwa zinapunguza mawazo kwani kwa uhalisia pombe haipunguzi mawazo.

"Vijana wanaotumia pombe wa kiwa na umri mdogo wanaweza kuathirika kiafya, kama vile kijana anaweza kupata ugonjwa wa Ini, kuathiri  ubongo na kumbukumbu pia anaweza kupata vidonda vyatumbo na hata kupunguza kinga za mwili dhidi ya magonjwa, kutokana na  matumizi ya vileo vikali.

Kwa upandewake Emmanuel Msigwa ambaye ni kijana wa Kata hiyo ,amesema  kuwa kutokana na utandawazi wa sikuizi vijana wengi hushawishika kutumia pombe kali wakiwa na umri mdogo wakidhani kuwa nisalama  kiafya.

"Baadhi ya vijana hutumia pombe pale wanapokuwa na msongo wa mawazo,wakiamini kuwa pombe ndio njia pekee ya kuondoa mawazo pia wengiwao hutumia pombe  kwa kuiga  makundi mabaya ya mtaani".

Huku Getruda  Bulinje ambaye ni mkazi wa kata ya kihesa,amesema  kuwa katika jamii yetu  vijana wengi hutumia pombe wakiwa na umri mdgo kutokana na kukosa malezi bora kwa wazazi, kwani hupelekea  vijana haokujiona wanacho kifanya nisahii.

"Kutokana na janga hili la vijana kutumia pombe husababisha athari kubwa katika jamii kana vile, vijana kuwa na tabia mbaya, mimba za utotoni kutokea,pia wengi wao hushawishika kuacha masomo pasipo kujua madhara yake".

Hivyo matumizi ya pombe kwa vijana wakiwa na umri mdogo huchangia vijan wengi kuporomoka kimaadili na wengine kushuka katika masomo kutokana na  matumizi ya pombe wakiwa naumri mdogo, licha ya hvyo wazazi na walezi wanapaswa kuwalea watoto katika  maadili bora.

Sponsored ads

Mid 1

Mid2

Ad3