HALI YA BIASHARA MSIMU WA MFUNGO
NA EASTER KAMETA(UoI)
MATUKIO DAIMA
Baadhi ya wafanyabiashara wa viungo vya chakula mkoani Iringa wameeleza juu ya hali ya biashara hisusani msimu huu wa mfungo wa kwaresma na ramadhani.
Wakizungumza na Matukio Daima Media wafanyabiashara wa viungo vya chakula amedai kuwa kwasasa wateja wameongezeka kutokana na matumizi ya futari jioni huku akitaja baadhi ya viungo kama pilipili , mdarasini ,iriki kuwa ni muhimu katika futari.
"Mahitaji ya viungo yanaongezeka sana katika kipindi hiki ambacho watu wengi walio funga wanahitaji viungo hasa katika maandalizi vyakula maalum wakati wa kufuturu jioni matumizi ya viungo kamaVitunguu Tangawizi, Kitunguu swaumu ,Pilipili ,Mdalasini, karafuu,na iriki uongezeka kwa sababu vyakula vya futari kama vile sambusa, supu, wali, nyama ."
Japhet Muhando ameeleza juu ya bei za viungo ambazo zimepanda kutokana na uhitaji wa watu pia ametaja kuwa bei hizi zimekuwa faida kwa wafanyabiashara wakubwa kwani inawapatia faida.
" Bei imepanda kutokana na ongezeko la uhitaji wa Vitunguu na tangawizi hivyo hufanya wafanyabiashara kupandisha bei hasa kipindi hiki cha mfungo pia Wafanyabiashara wa jumla hupata wateja wengi Kutoka sehemu mbalimbali kama vile mahotelini, mama lishe, wauza futari hivyo hufanya wao kupata faida"
Vilevile Jenister Mlelwa amesema kuwa ushindani umeongezeka kutokana na kwamba baadhi ya wananchi wanapenda kufanya biashara za mda mfupi ili kuweza kujipatia faida kubwa pia huku akutaja kuwa wengine hukosa faida kutokana na mitaji midogo.
"Ushindani unaongezeka kwa sababu watu wengi huingia katika biashara ya muda mfupi ili kuwezakupata faida kubwa hasa vijana ,Mama lishe, Wafanyabiashara wadogo hali hii husababisha kushuka kwa faida kwa wafanyabiashara ambao ni wadogo pia kupoteza mitaji yao kutoka na watu wengi kuuza bidhaa aina moja katika sehemu moja."
shizya Mmbwaga ameeleza juu ya utunzaji wa viungo vya chakula kuwa ni mgumu hasa msimu huu wa mvua ,pia ametaja kuwa upatikanaji wake ni mgumu kwa baadhi ya viungo na kupelekea wafanyabiashara wengi kuchukua bidhaa nyingi hadi hupelekea kuadimika sokoni .
"Utunzaji wa viungo vya chakula msimuu huu wa mvua ni mgumu pia upatikanaji mgumu kwani baadhi ya bidhaa hupatikana kwa msimu hivyo hufanya wauzaji wengi hukimbilia kununua kwa wakati mmoja bidhaa ambapo hupelekea kuadimika kwa haraka sokoni ,hali hii hupelekea watu wenye mtaji mdogo kukosa uhakika wa bidhaa pia biashara zao kuyumba"
