Kwa Habari za kitaifa, Kimataifa, Michezo, Burudani,Uchambuzi na matangazo. Matukio Daima Blog, Ni yetu Sote!
MAKAMU WA RAIS BALOZI NCHIMBI AZINDUA MFUMO WA KUTABIRI KIASI CHA MAJI KWENYE MITO

MAKAMU WA RAIS BALOZI NCHIMBI AZINDUA MFUMO WA KUTABIRI KIASI CHA MAJI KWENYE MITO

 


📌Azitaka taasisi za Serikali kujenga ushirikiano na sekta binafsi katika kukabiliana na changamoto ya maji

Na Lilian Kasenene, Morogoro

Matukio Daima Media

MAKAMU  wa Rais Balozi Dk Emmanuel Nchimbi ameitaka wizara ya maji na taasisi zote za Serikali kujenga mtandao wa ushirikiano na sekta binafsi kutatua changamoto zinazoikabili sekta hiyo huku akiwahimiza wadau wa maendeleo kulinda na kutunza vyanzo vya maji ili kwenda sambamba na dhamira ya rais ya kumtua mama ndoo kichwani.


Dk Nchimbi alisema hayo mjini Morogoro wakati wa  maadhimisho kilele cha wiki ya maji kitaifa na siku ya maji Duniani.

Dk Nchimbi alisema kauli mbiu ya maadhimisho ya siku ya maji duniani, isemayo "maji na jinsia" imekuja wakati muafaka kwani wanawake wamekuwa waathirika wakubwa kiusalama kutokana na changamoto za maji ambapo asilimia tano ya hasara inayopatikana duniani, karibu dola bilioni 170 inatokana na kukosekana maji .

"Wanawake Wana mchango wa kipekeebama shida ama Raha katika maji ni zaidi ya asilimia 60 wamekuwa watu wa maji usiku na mchana katika changamoto ya na utunza familia,",alisema.


Alisema hadi sasa vijiji 10, 758  vimefikiwa na maji safi na salama ambapo bado vijiji 1575 havijafikiwa huku wizara hiyo imeshaweka mikakati ya kuvifikia

Makamu huyo wa Rais alisema  kupitia sera ya maji ya mwaka 2022 Tanzania imepata mafanikio ambapo  asilimia 92.5 ya Watanzania waishio mjini  na asilimia 85.2 wanapata maji safi na salama .

Alisema katika Dira ya maendeleo ya Taifa 2050  inakadiriwa kuwa idadi ya watu itaongezeka  hadi kufikia watu milioni 118 wengi wao wakiwa ni wa maeneo ya mijini ambapo itazalisha changamoto nyingi zikiwemo Elimu, chakula, Afya, Ajira na kubwa zaidi ni Maji.

"Ni muhimu kulinda na kutunza vyanzo vya maji, na uwekezaji  uzingatie sera na dira ya maendeleo ya Taifa,"alisema.

Aifha alisema nia ya Serikali ni kuona mpango wa gridi ya maji ya Taifa inafanikiwa, sambamba na kufungwa kwa mita janja ili kumfanya mtumiaji awajibike na kuzuia upotevu wa maji.

Alisisitiza kubuni vyanzo vipya vya mapato badala ya kutegemea vilivyopo ili kukuza sekta ya maji na kuimarisha huduma za usafi wa mazingira ikiwemo kudhibiti mfumo wa maji taka usiingiliane na mfumo wa maji safi na kuleta madhara kwa watumiaji.

Kabla ya kuwahutubia wananchi katika viwanja vya mkwawa Leaf, mkoani hapa Makamu wa Rais alitembelea bwawa la Mindu linalotegemewa kama chanzo kikuu cha maji na zaidi ya asilimia 75 ya wananchi wa mji wa Morogoro ambapo amezindua mfumo wa utabiri wa kiasi cha maji kwenye mito Tanzania, pamoja na kupanda mti.


Awali  mkurugenzi wa bodi ya maji Bonde la Wami Ruvu  Eibariki Mmasi  alisema  mfumo huo wa utabiri  wa kiasi cha maji  kwenye mito Tanzania utakuwa na uwezo kutabiri yatakayotokea kwenye mito hiyo ndani ya siku kumi hadi miezi mitatu na hivyo kurahisisha kuchukua hatua za haraka na uhakika kutokana na hali ya mabadiliko ya tabia ya nchi.

Uzinduzi huo umefanyika katika la Bwawa la Mindu Mjini Morogoro ambako amejionea namna Wizara ya Maji inavyoshiriki katika utunzaji, ulinzi na Uendelezaji wa Rasilimali za Maji.

Mhandisi Mmasi alisema mfumo huo ni Moja ya jitihada za Wizara ya Maji kuhakikishia inaondoa changamoto za Sekta kwa kuwezesha upatikanani wa taarifa sahihi za kiwango cha Maji.

Alisema Bwawa hilo ni sehemu ya maeneo yatakayonufaika na changamoto hiyo kwani linapokea maji kutoka sehemu mbalimbali za nchi

Waziri wa Maji  Jumaa Aweso, aliahidi wizara yake kutokuwa kikwazo cha upatikanaji wa maji kwa  wananchi na kwamba sasa hakuna mtendaji atakayekaa ofisini.

"Katika Suala la maji Rais anataka matokeo, wewe makamu wa Rais wewe na waziri mkuu mnataka matokeo, sisi viongozi wa wizara hatutawaangusha na tunaahidi kutokuwa kikwazo kwenu na kwa Watanzania"alisema.


Naye Mwakilishi wa sekta binafsi mhandisi Ngwisa Mpembe, alisema  Sekta binafsi hiyo iko tayari kushirikiana na Serikali ambapo hadi sasa wamefanya uwekezaji wa zaidi  ya shilingi Trilioni 1.2  kwenye sekta  maji.

Alisema uwekezaji huo ni pamoja ujenzi wa viwanda vya mabomba ya maji, vifaa vya ujenzi vya maji, mita jinja na wamekusudia kuboresha zaidi katika teknolojia , Rasilimali watu na kutengeneza wztaalam wa ndani. 


Aliahidi kuendelea kushirikiana na Serikali katika kuwekeza ,kufanya ubunifu , ujenzi wa miundombinu , teknolojia, usafi wa mazingira, kulinda vyanzo vya maji na upatikanaji wa fedha ili kuhakikisha kunakuwa na upatikanaji wa maji kwa wote.

Spika wa Bunge la Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mussa Hassan Zungu alisema  Bunge  litahakikisha linaunga mkono masuala yote yanayopelekwa bungeni yanayohusiana na maji.

Alisema wizara ya Maji inaleta matumaini makubwa kwa  Watanzania na kwamba hivi karibuni changamoto ya maji  itaisha kutokana na hatua zinazochukuliwa na wizara hiyo.

Alimpongeza Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hasani kwa kutekeleza mradi wa bwawa la Kidunda lililopo mkoani Morogoro ambalo tangu mwaka 1954 lilianza  kuzungumziwa.



Sponsored ads

Mid 1

Mid2

Ad3