Kwa Habari za kitaifa, Kimataifa, Michezo, Burudani,Uchambuzi na matangazo. Matukio Daima Blog, Ni yetu Sote!
BODABODA AUAWA KWA KUCHOMWA KISU

BODABODA AUAWA KWA KUCHOMWA KISU

 

Na Fadhili Abdallah,Kigoma 


Polisi Mkoa wa Kigoma inafanya  uchunguzi wa  kifo cha Joseph Gidion Filimon (30) dereva pikipiki na mkazi wa Mlole Manispaa ya Kigoma Ujiji aliyeuawa kwa kuchomwa na kisu eatu wasiojulikana.


Awali wananchi wanaoishi jirani na marehemu walimtuhumu mwanamke aliyekuwa akiishi na bodaboda huyo ambaye anaelezwa kumfikisha marehemu Hospitali y rufaa ya mkoa Kigoma Maweni na baadaye kutoweka huku akizima simu zake zote.


Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kigoma, Filemon Makungu akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake mjini Kugoma alisema kuwa  uchunguzi unaendelea ili kubaini chanzo halisi cha tukio hilo, huku akitoa wito kwa yeyote mwenye taarifa muhimu kujitokeza kusaidia uchunguzi huo.


Akizungumzia tulio hilo Baba mzazi wa marehemu, Gidion Philemon amesema familia imeachwa na maswali mengi, akieleza kuwa mwanamke aliyekuwa akiishi na mwanawe alimfikisha hospitalini kisha kutoweka kusikojulikana na hazipatikani hadi sasa na simu zake zimezimwa.


 Mzee Philemoni  alisema kuwa  alipigiwa simu na mwanamke huyo akielezwa kuwa mwanawe alichomwa na kitu nyenye ncha kali  kwenye Bega lake la kulia na  watu wasiojulikana ambo linalozua utata zaidi kuhusu tukio hilo.



Sponsored ads

Mid 1

Mid2

Ad3