Kwa Habari za kitaifa, Kimataifa, Michezo, Burudani,Uchambuzi na matangazo. Matukio Daima Blog, Ni yetu Sote!
SERIKALI YA LIPA DENI LA MIFUKO YA HIFADHI YA JAMII NCHINI

SERIKALI YA LIPA DENI LA MIFUKO YA HIFADHI YA JAMII NCHINI

 


Na,Jusline Marco;Arusha

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Ajira na Mahusiano, Mheshimiwa Deus  Sangu, amesema hadi sasa Serikali imefanikiwa kulipa asilimia 95 ya deni la mifuko ya hifadhi za jamii nchini ambalo lilirithiwa kabla ya mwaka 1999, hatua ambayo imesaidia kuimarisha ukwasi na ufanisi wa mifuko hiyo katika kuwahudumia wanachama.


Akizungumza jijini Arusha wakati wa uzinduzi wa Sera ya Taifa ya Kinga ya Jamii ya Mwaka 2023, Waziri Sangu ametoa shukrani za dhati kwa Serikali ya Awamu ya Sita kwa utaratibu wake wa kishujaa wa kulipa deni Hilo la kihistoria la shilingi trilioni 4.46 lililokuwa linaikabili mifuko hiyo  ya hifadhi ya jamii nchini. 


Mhe. Sangu ameeleza kuwa hatua hiyo ni sehemu ya maboresho ya Sekta ya Kinga ya Jamii yaliyoanza mwaka 2018 kwa lengo la kutekeleza Ibara ya 11 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, inayoiagiza mamlaka kuweka taratibu za kusaidia wananchi wakati wa uzee, maradhi na ulemavu.


Amesisitiza kuwa kulipwa kwa madeni hayo kumeongeza kasi ya ulipaji wa mafao kwa wakati na kuleta utulivu wa kiuchumi kwa wastaafu, huku kukiakisi dhamira ya dhati ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan katika kuwajali wananchi wake na kulinda haki zao za msingi.


Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Arusha Joseph Mkude akizungumza katika Mkutano huo kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Arusha CPA Amos Makalla ameeleza kuwa kufanyika kwa mkutano huo wenye kauli mbiu ya "Kinga ya jamii kwa wote msingi wa maendeleo" ni sehemu ya mafanikio ya serikali kwani kinga ya jamii ni suala muhimu kwa maendeleo ya Taifa na imekuwa ikigusa makundi mbalimbali ndani ya jamii.

Sponsored ads

Mid 1

Mid2

Ad3