Kwa Habari za kitaifa, Kimataifa, Michezo, Burudani,Uchambuzi na matangazo. Matukio Daima Blog, Ni yetu Sote!
ALIYETABIRI MWISHO WA DUNIA MWAKA 2025 GHANA AKAMATWA NA POLISI

ALIYETABIRI MWISHO WA DUNIA MWAKA 2025 GHANA AKAMATWA NA POLISI




Jeshi la Polisi la Ghana limethibitisha kukamatwa kwa "Nabii Bandia" Evans Eshun, anayejulikana zaidi kwa jina la Ebo Noah. 

Ebo Noah alitangaza kwa wafuasi wake kwamba alipata maono ya Mungu kuwa mafuriko makubwa ya dunia yatatokea kuanzia 25 Desemba 2025, yatakayodumu kwa miaka mitatu hadi minne, na kwamba tu wale watakaokua kwenye "safina" zake wataokolewa. 

Alitia misingi hii kwa mfano wa Noa wa Biblia, akijenga "safina" za kuni kwa ajili ya wokovu Siku iliyotarajiwa ya kuanza kwa mafuriko (25 Desemba 2025), mafuriko hayo hayakusikika kutokea. 

Ebo Noah baadaye alitangaza kwamba Mungu alikuwa ameongeza muda na alikuwa ametoka na "maono mapya" ya kuendelea kujenga zaidi "safina." 

Kuna ripoti kwamba baadhi ya wafuasi walimchangoa pesa, na kisha Ebo Noah alionekana akitumia pesa hizo kununua gari la kifahari (Mercedes-Benz), jambo lililosababisha madai ya utapeli na mbinu ya kuchukua pesa kwa wafuasi.

 Wanasheria Ghana wameweka wazi kwamba utabiri ulioshindwa na ujenzi wa safina bila vibali unaweza kumletea Ebo Noah mashitaka ya kisheria, ikiwa ni pamoja na ukiukaji wa sheria za ujenzi wa meli na usambazaji wa habari potofu zinazoweza kusababisha hofu ya umma

Sponsored ads

Mid 1

Mid2

Ad3