SABABU ZA AJALI BARABARANI ZATAJWA IRINGA
NA EASTER KAMETA (UoI)
MATUKIO DAIMA (UoI)
Maafisa isafirishaji mkoa wa Iringa wataja baadhi ya njia zitakazo saidia ili kuepusha Wimbi kubwa Ajali za barabarani
Matukio daima imezugumza na moja ya maafisa usafilishaji wa vyombo vya moto Given Marcus ameeleza kuwa madereva wote wanapaswa kuzingatia usalama wa magari yao kabla ya kuanza safari , amewataka madeleva kuwa makinina kufuata sheria za barabarani.
"Madeleva wote wanapaswa kuzingatia usalama wa magari yao kabla hawajatoka stendi pia kuzingatia ukaguzi wa magari yao mara kwa mara pia unahitajika umakini wa hali ya juu awapo barabarani kwani ankua mebeba roho za watu ,kufuata sheria za barabarani kama vile zebra na taa za barabara ni muhimu kwani inasaidia kuepusha ajali zisizo za razima."
Kwaupande wake Daudi Sanga meeleza kuwa maegesho ya vyombo vya moto yamekuwa changamoto kubwa kwani baadhi ya watu na kutaja kuwa baadhi ya watu hufanya maegesho katika pembe za barabara pia amewataka madeleca bajaji na bodaboda kufuata sheria.
"Madereva bodaboda na bajaji wanekuwa chachu ya kusababisha ajali kwani wao huwa wana lazimisha kupitasehemu ambayo ni ndogo ,hafuati Sheria kwani wao hupita hata kama taa ziwe hazija ruhusu ambapo hali hii huweza kupelekea ajari kea mtumiaji wa barabara anayetembea kea miguu pia baadhi ya madeleva wamekuwa na tabia ya kuegesha vyombo vyao vya moto barabarani hivyo hupelekea kutokea kwa ajali"
Frank Mwaibunga ameeleza kuwa Vijana wengi wanaendesha vyombo vya usafiri kwa mihemko na mashindano huku akutaja kuwa hali hii hutokana na kukosekana kwa elimu juu ya matumizi ya vyombo vya moto.
" Baadhi ya madeleva hawana elimu ya kutosha juu ya matumizi sahihi ya vyombo vya moto hivyo hupelekea wao kutumia vyombo hivyo kwa kasi ya hali ya juu nakupekekea kutokea kwa ajali barabarani pia wanao endesha vyombo hivyo wengi wao ni vijana wadogowadogo hivyo huendesha kwa mashindano kutokana hawana elimu hivyo hua wao ni chanzo cha ajali hizo."
John Mbunda ameeleza kuwa baadhi ya madeleva hutumia vilevi kabla ya safari pia ametaja kuwawengine huendesha vyombo vya moto wakiwa wamechoka na wengine wakiwa na mawazo ambapo si sahihi.
"Matumizi ya vilevi kwa baadhi madereva kabla ya kuanza safari huku wakidai kuwa wakifanya hivyo inawasaidia katika kujiamini jambo ambalo si sahihi pia madereva wengine huendesha vyombo vya usafiri wakiwa wamechoka ambapo hali hii huweza kufanya kutokea kwa ajali kutokana kwamba mwili na akili haviko tayari kufanya kazi lakini mtu analazimisha piawengine huendesha magari wakiwa na msongo wa mawazo na kupelekea ajali."


