LEMA AMCHOKONOA MCHUNGAJI MSIGWA
NA MATUKIO DAIMA MEDIA
KATIKA kinachoonesha ni choko choko za Mwanasiasa maarufu nchini kupitia chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Godbles Lema dhidi ya aloyekuwa kada wa chama hicho kabla ya kuhamia Chama cha Mapinduzi (CCM) Mchubgaji Peter Msigwa ni juu ya ujumbe wake alioandika kupitia page yake ya Instagram kuwa Msigwa bado anasubiri kuwa DC.
Hapa chini ni ujumbe ulioandikwa na Lema kwenye ukrasa wake wa Instagram ⬇️⬇️⬇️
"Mungu aliwasamehe makahaba, lakini ulipofika wakati wa kumchagulia Mwanawe mama, alimchagua bikira. Jifunze kutoka kwa Mungu ,Bado unasubiri kuwa DC? Sababu ya kurudi ni mauaji 29/10/2025 kwani ina nguvu na heshima zaidi ya ile sababu iliyokuondoa kwenye wajibu mwema."
Hata hivyo ukweli na kwamba Mchungaji Msigwa kwa sasa ametingwa na kusimamia miradi yake na hata ushiriki wake kwenye siasa za CCM umekuwa mdogo tofauti na ilivyokuwa kabla ya uchaguzi mkuu mwaka 2025.

