Kwa Habari za kitaifa, Kimataifa, Michezo, Burudani,Uchambuzi na matangazo. Matukio Daima Blog, Ni yetu Sote!
KATIBU CHADEMA RUNGWE ASHIKILIWA KWA TUHUMA ZA UCHOCHEZI.

KATIBU CHADEMA RUNGWE ASHIKILIWA KWA TUHUMA ZA UCHOCHEZI.

 

Polisi Mkoa wa Mbeya imemkamata Award Karonga, Mkazi wa Katumba wilaya ya Rungwe mkoani Mbeya ambaye ni Katibu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Wilaya ya Rungwe akituhumiwa kwa makosa ya kichochezi.


Kamanda wa Polisi mkoa wa Mbeya Kamishna msaidizi mwandamizi wa Polisi SACP Benjamin Kuzaga, kupitia taarifa yake kwa umma, amesema mtuhumiwa alikamatwa Januari 29, 2026 saa 4 asubuhi katika eneo la Katumba, Kata ya Ibighi Tukuyu Wilaya ya Rungwe kwa tuhuma mbalimbali za kijinai ikiwepo uchochezi.


Polisi Mbeya imesema upelelezi wa shauri hilo unaendelea na ukikamilishwa hatua zaidi za kisheria zitachukuliwa dhidi ya mtuhumiwa huyo.


Sponsored ads

Mid 1

Mid2

Ad3