UGONJWA WA MOYO TISHIO KWA JAMII -DKT HERY MWANDOLELA
Na Angelina Mbunda(UoI) MATUKIO DAIMA
Takribani watu milioni Ishirini wanafariki kwa mwaka mmoja kutokana na magonjwa ya moyo yanayosbabishwa na kukaa kwa muda mrefu bila ya kusimama.
Akizungumza katika kipindi cha Asubuhi ya Moto kilichorushwa na Matukio Daima Media jana Mkurugenzi wa Hopsitali ya Heameda Dkt Herry Mwandolela ambaye pia ni Daktari wa Magonjwa ya moyo amesema kuwa kutokana na takwimu za mwaka Jana zinaonesha kuwa watu wengi wanakufa kutokana na ugonjwa wa moyo unaosababishwa na kukaa kwa muda mrefu bila ya kusimama."Kwa takwimu za mwaka Jana zinaonesha takribani watu milioni Ishiri wanafariki ndani ya mwaka mmoja kwa ugonjwa wa moyo ambao unatokana na kukaa kwa muda mrefu bila ya kusimama".
"Pia vipo viashiria vingi ambavyo mtu akiwa anakaa kwa muda mrefu bila ya kusimama atapata ugonjwa wa moyo japo kuwa anaweza akapata na magonjwa mengine Kama vile kisukari, na saratani.
Hivyo anapaswa kujua changamoto haiji kwa haraka HUwa inakuja taratibu Sana na inaweza kumpata mtu miaka kadhaa mbele".
Naye Caedmon Mtweve amesema kuwa ugonjwa wa moyo hautokani na kukaa kwa muda mrefu tu vile vile ulaji wa vyakuae vyenye mafuta mengi vinaweza kusababisha ugonjwa wa moyo.TAZAMA VIDEO HII BOFYA LINK
"Ulaji wa vyakula vyenye mafuta mengi vinaweza kuathiri moyo kwasababu mafuta yanaenda kuganda kwenye mishipa ya damu na kusababisha dam kuto kufanya kazi vizuri".
Hivyo kutokana na kuendelea kwa magonjwa ya moyo hatuna budi kutafuta nafasi ya kufanya mazoezi walao Kila siku ata dakika chahe ili tuweze kuepuka ugonjwa huo wa moyo ilo hasa wafanyakazi wa maofisini na madreva wa magari ya habiria na mozigo.TAZAMA HAPA FULL VIDEO BOFYA LINK HII
Kwa ushauri wa Kiafya wasiliana na Dkt Hery Mwandolela kwa namba 0758012006

